Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Simon Songe Lusengekile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busega

Primary Question

MHE. SIMON S. LUSENGEKILE aliuliza: - Je ni lini ahadi ya Rais wa Awamu ya Tano ya kuipandisha hadhi Shule ya Sekondari Nassa itatekelezwa?

Supplementary Question 1

MHE. SIMON S. LUSENGEKILE: Mheshimiwa Naibu Spika, naishukuru Serikali kwa majibu yake awali, lakini nina swali moja la nyongeza.

Kwa kuwa, Halmashauri ya Wilaya ya Busega ni moja ya Halmashauri mpya hapa nchini na makusanyo yake ni kidogo sana.

Je, Serikali haioni sababu ya msingi ya kutenga fedha kutoka Serikali Kuu ili kuanza ujenzi wa miundombinu hii ambayo Mheshimiwa Waziri ameitaja?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Simon Songe Lusengekile, Mbunge wa Jimbo la Busega kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza Mkurugenzi afanye tathmini kubaini gharama zinazohitajika kujenga madarasa hayo na miundombinu hiyo na awasilishe rasmi Ofisi ya Rais – TAMISEMI ili tuweze kuona kama Halmashauri inaweza kujenga sehemu ya miundombinu hiyo, lakini eneo lingine la miundombinu, Serikali Kuu iweze kuchukua. Ahsante.

Name

Mussa Ramadhani Sima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Mjini

Primary Question

MHE. SIMON S. LUSENGEKILE aliuliza: - Je ni lini ahadi ya Rais wa Awamu ya Tano ya kuipandisha hadhi Shule ya Sekondari Nassa itatekelezwa?

Supplementary Question 2

MHE. MUSSA R. SIMA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Singida Mjini tumekarabati na kujenga shule ya Sekondari ya Mungumaji na kila kitu kiko tayari na tumeomba ili kuweze kupandishwa hadhi kuwa Kidato cha Tano na Sita lakini mpaka sasa kibali hicho hakijatoka.

Je, ni lini Serikali itatoa kibali cha kuhakikisha sasa tunaanza shule ya Kidato cha Tano na Sita pale Mungumaji Sekondari?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mussa Sima, Mbunge wa Jimbo la Singida Mjini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ninampongeza Mheshimiwa Sima na Manispaa ya Singida Mjini kwa kufikia hatua hiyo kukamilisha vigezo vinavyohitajika na nimhakikishie Ofisi ya Rais TAMISEMI, tumelichukua hili na baada ya hapa nitafuatilia nione wapi tumekwama ili shule zianze huduma mapema. Ahsante.

Name

Saashisha Elinikyo Mafuwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hai

Primary Question

MHE. SIMON S. LUSENGEKILE aliuliza: - Je ni lini ahadi ya Rais wa Awamu ya Tano ya kuipandisha hadhi Shule ya Sekondari Nassa itatekelezwa?

Supplementary Question 3

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Shule ya Sekondari Lemira ina hekta 20 lakini ina madarasa toshelevu kabisa ya kuweza kuanzisha Kidato cha Tano na cha Sita.

Je, ni lini Serikali itaipandisha hadhi shule hii ya Lemira kuwa Kidato cha Tano na cha Sita?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Saashisha Mafuwe, Mbunge wa Jimbo la Hai kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, nimuombe Mheshimiwa kufuatilia kama Halmashauri ya Hai imekwishawasilisha maombi hayo kwa Kamishina wa Elimu lakini baada ya kupata ripoti ya Mdhibiti wa Kanda wa Elimu. Kama hiyo imekwishafanyika, nitawasiliana na yeye baada ya Kikao hiki ili tuweze kuona namna gani tunalisukuma hili liweze kukamilika mapema.

Name

Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Primary Question

MHE. SIMON S. LUSENGEKILE aliuliza: - Je ni lini ahadi ya Rais wa Awamu ya Tano ya kuipandisha hadhi Shule ya Sekondari Nassa itatekelezwa?

Supplementary Question 4

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi, tofauti na shule ya Changarawe ambayo Serikali mmekuwa mkitusaidia sana. Shule ya JJ Mungai ambayo ni ya Kidato cha Kwanza mpaka cha Sita kimekuwa na uhitaji wa mabweni na uboreshaji wa miundmbinu yake.

Je, Serikali mko tayari kutusaidia kama mlivyofanya shule ya sekondari Changarawe?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Cosato Chumi, Mbunge wa Jimbo la Mafinga Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, majengo yetu au miundombinu yote katika shule zetu kwanza tunayo bajeti ya kumalizia majengo ambayo yameanzishwa na wananchi kwa maana ya maboma, kwa kutumia EP4R na tumeendelea kufanya katika miaka yote na mwaka huu pia. Pia kwa sekondari tunayo bajeti ya SEQUIP lakini tunakwenda kutekeleza mpango wa BOOST. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba katika eneo hilo kwanza tutakwenda kuona majengo yanayohitajika, lakini tuone gharama zake, kwa kushirikiana na mapato ya ndani ya Mji wa Mafinga na Ofisi ya Rais TAMISEMI itaona namna gani tunaweza tukatoa fedha kwa ajili ya kazi hiyo.(Makofi)