Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 46 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 403 2022-06-17

Name

Jacquline Andrew Kainja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HAMIS M. MWINJUMA K.n.y MHE. JACQUELINE K. ANDREA aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itatoa fedha kukamilisha ujenzi wa Shule katika Kijiji cha Izengabatogilwe, Kata ya Ugalla - Urambo?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Jaqueline Andrea Kainja, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, katika mwaka wa fedha 2021/2022 Serikali kupitia Mpango wa Maendeleo kwa Ustawi wa Taifa na Mapambano Dhidi ya UVIKO-19 imepeleka Shilingi Milioni 40 kwa ajili ya ujenzi wa vyumba viwili vya madarasa katika kitongoji cha Gimagi kwenye shule shikizi ya shule Mama ya Izengabatogile.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika mwaka wa fedha 2022/2023, Serikali imetenga Shilingi Milioni 220 kwa ajili ya ukamilishaji wa maboma ya madarasa yaliyojengwa kwa nguvu za wananchi katika Halmashauri ya Wilaya ya Urambo.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali itaendelea kutenga fedha kwa ajili ya ukamilishaji wa maboma ya madarasa ikiwemo ya shule katika Kijiji cha Izengabatogile, Kata ya Ugalla, Wilayani Urambo.