Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Hamis Mohamed Mwinjuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muheza

Primary Question

MHE. HAMIS M. MWINJUMA K.n.y MHE. JACQUELINE K. ANDREA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itatoa fedha kukamilisha ujenzi wa Shule katika Kijiji cha Izengabatogilwe, Kata ya Ugalla - Urambo?

Supplementary Question 1

MHE. HAMIS M. MWINJUMA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri. Kwenye Jimbo la Muheza, Serikali iliahidi kupeleka Shilingi Milioni 600 kwa ajili ya shule mbili za sekondari kwenye Kata mpya. Kata moja ya Makole haijapata hata shilingi moja mpaka hivi tunavyoongea na mwaka wa fedha unakaribia kuisha.

Je, Serikali ina mpango wowote wa kupeleka fedha hizi kama ilivyoahidi?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Hamis Mwinjuma, Mbunge wa Jimbo la Muheza kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ujenzi wa sekondari mpya katika Kata ambazo hazina sekondari unaendelea na kwa awamu ya kwanza Serikali ilipeleka Shilingi Milioni 470 katika Kata hizo, na itakwenda kumalizia Shilingi Milioni 130 kukamilisha Milioni 600. Ninamhakikishia Mheshimiwa Mbunge kama Kata hii ya Makole haipo kwenye orodha ya kupata Milioni 600 na haijapata, tutafuatilia tuone ni kwanini haijapata ili iweze kupata kama ipo kwenye orodha ya kupata shule hizo.(Makofi)

Name

Cecilia Daniel Paresso

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HAMIS M. MWINJUMA K.n.y MHE. JACQUELINE K. ANDREA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itatoa fedha kukamilisha ujenzi wa Shule katika Kijiji cha Izengabatogilwe, Kata ya Ugalla - Urambo?

Supplementary Question 2

MHE. CECILIA D. PARESSO: Mheshimiwa Naibu Spika, ninakushukuru kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika Halmashauri zetu mbalimbali hapa nchini kuna nguvu za wananchi zimetumika kujenga shule kwenye level ya shule za msingi na shule za sekondari, zimebaki kama maboma kwa muda mrefu bila ukamilishaji.

Je, Serikali sasa kwanini isizitake Halmashauri, izitambue na kuwapa timeframe wa ukamilishaji wa majengo hayo ambayo ni nguvu za wananchi?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Cecilia Paresso, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba Serikali kwa nia njema ya kuhakikisha kwamba maeneo yetu yote yanakuwa na shule za msingi kwa maana ya vijiji lakini na shule za sekondari kwenye Kata, ilihamasisha nguvu kazi za wananchi lakini Serikali inachangia nguvu zile kukamilisha maboma ya madarasa.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imefanya kazi kubwa sana, sote ni mashahidi kwamba fedha nyingi sana zimetolewa kwa ajili ya kukamilisha madarasa hayo katika miaka yote ya fedha ukiwepo mwaka huu, kupitia EP4R, kupitia SEQUIP lakini tunakwenda na mpango wa BOOST.

Mheshimiwa Naibu Spika, pia tunafahamu kwamba tungependa kuweka deadline kukamilisha maboma hayo kwa Halmashauri, lakini pia bado kuna changamoto za uwezo wa mapato ya ndani kukamilisha kwa pamoja kutoka na wingi wa majengo ambayo yamejengwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba safari ni hatua, tumekwenda kwa kiasi kikubwa sana na tutakwenda kukamilisha maboma yaliyokamilika, kwa sababu mpango umewekwa vizuri kwa ajili ya shughuli hiyo.