Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 46 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 405 2022-06-17

Name

Soud Mohammed Jumah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Donge

Primary Question

MHE. MOHAMED JUMAH SOUD aliuliza: -

Je, ni vigezo gani hutumika kuanzisha Vituo vya Polisi maeneo yenye idadi kubwa ya watu pamoja na vitendo vya uhalifu?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mohamed Jumah Soud, Mbunge wa Donge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, vigezo vinavyotumika kuanzisha Vituo vya Polisi ni ongezeko la watu, ongezeko la matukio ya uhalifu, umbali kati ya Kituo kimoja cha Polisi na kingine, uwepo wa miundombinu ya Serikali, shughuli za kibiashara pamoja na maeneo ya kimkakati kwa ajili ya ulinzi na usalama wa nchi, uwezo wa kibajeti na utayari wa wananchi na Mamlaka zao za Serikali za Mitaa ni vigezo vingine tunavyovitumia. Hatua inayofuata ni mapendekezo ya uanzishwaji wa kituo husika kuwasilishwa kwenye Kamati ya Usalama ya Wilaya, Kamati ya Usalama ya Mkoa na kisha ushauri wao huwasilishwa kwa Mkuu wa Jeshi la Polisi kwa ajili ya utekelezaji. Nashukuru.