Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Soud Mohammed Jumah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Donge

Primary Question

MHE. MOHAMED JUMAH SOUD aliuliza: - Je, ni vigezo gani hutumika kuanzisha Vituo vya Polisi maeneo yenye idadi kubwa ya watu pamoja na vitendo vya uhalifu?

Supplementary Question 1

MHE. MOHAMED JUMAH SOUD: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri nina swali la nyongeza. Kwa kuwa Jimbo la Donge limepanuka sana na hivyo vigezo ambavyo amevizungumza Mheshimiwa Naibu Waziri vingi vyake vinakidhi kuanzishwa Kituo cha Polisi katika Jimbo la Donge na halikadhalika uharamia umeongezeka sana kiasi kwamba mazao sasa hivi kulima kumekuwa ni shida, mifugo kufuga imekuwa ni tabu. Swali hili niliwahi kuuliza hapa na Mheshimiwa Naibu Waziri aliniahidi kwamba atafanya tathmini ili kuangalia uwezekano wa utekelezaji. Sasa je, ananiahidi vipi ile tathmini imeshafanyika na kama haijafanyika basi lini itakamilika ili utekelezaji uanze. Ahsante sana.

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la moja la nyongeza la Mheshimiwa Soud, kama ifutavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba kama nilivyosema ameeleza hapa Jimbo la Donge linakidhi vigezo hivyo, kupitia Bunge lako Tukufu nimwelekeze Kamishna wa Polisi wa Zanzibar na Wasaidizi wake waweze kufanya tathmini ya eneo hilo. Wakibaini kwamba linakidhi vigezo, basi hatua za kujenga Kituo cha Polisi liweze kufanyika. Mheshimiwa Mbunge tutapeana ushirikiano ili kuona kwamba jambo hilo linafanyika. Ahsante sana.