Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 46 Works and Transport Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 406 2022-06-17

Name

Dr. Faustine Engelbert Ndugulile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigamboni

Primary Question

MHE. DKT. FAUSTINE E. NDUNGULILE aliuliza:-

Je, ni kiasi gani cha fedha kimekusanywa tangu Daraja la Nyerere lianze kutumika na ni lini huduma ya daraja hili itatolewa bila malipo?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Faustine Engelbert Ndungulile, Mbunge wa Kigamboni, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kulifahamisha Bunge lako Tukufu kuwa Mfuko wa NSSF ulianza kupokea fedha zitokanazo na tozo kwa watumiaji wa Daraja la Nyerere mnamo tarehe 14 Mei, 2016 baada ya kuzinduliwa. Hadi kufikia mwishoni mwa mwezi Mei, 2022, Mfuko ulikuwa umekusanya jumla ya shilingi bilioni 66.86.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imeendelea kupunguza tozo kwa watumiaji wa daraja hilo tangu kuzinduliwa kwake kwa kuzingatia tathmini ya uwezo wa wananchi kumudu tozo hizi. Kwa mara ya mwisho, Serikali imepunguza tozo husika tarehe 21 Mei, 2022. Ahsante.