Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 13 Sitting 4 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 47 2023-11-03

Name

Vita Rashid Kawawa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Primary Question

MHE. VITA R. KAWAWA aliuliza:-

Je, lini Serikali itapeleka Walimu kukidhi mahitaji katika Shule za Sekondari na Msingi Wilayani Namtumbo?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Vita Rashid Kawawa, Mbunge wa Jimbo la Namtumbo kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imekuwa ikiajiri walimu wa Shule za Msingi na Sekondari kwa awamu kwa kuzingatia upatikanaji wa fedha. Katika mwaka wa fedha 2022/2023 na 2021/2022, Serikali iliajiri walimu 22,930 ambapo walimu 111 walipangiwa katika shule zilizopo kwenye Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali itaendelea kupeleka walimu kwenye Shule za Msingi na Sekondari zikiwemo zilizopo katika Wilaya ya Namtumbo kulingana na uhitaji lakini pia kulingana na upatikanaji wa fedha, ahsante.