Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Vita Rashid Kawawa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Primary Question

MHE. VITA R. KAWAWA aliuliza:- Je, lini Serikali itapeleka Walimu kukidhi mahitaji katika Shule za Sekondari na Msingi Wilayani Namtumbo?

Supplementary Question 1

MHE. VITA R. KAWAWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa fursa hii kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Kwa kuwa uwiano wa idadi ya walimu tuliopata katika shule za msingi na sekondari haulingani na walimu waliofariki, waliostaafu na waliohama kwa vibali vya TAMISEMI hivyo kufanya uhaba mkubwa kuendelea kuwepo.

Je, Serikali inaweza kutupa kipaumbele wilaya za pembezoni ikiwemo Namtumbo kutuongezea idadi ya walimu wakati inagawa walimu hao? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; kwa kuwa shule za msingi za Namtumbo tuna walimu 867 na tuna upungufu wa walimu 418; je Serikali inaweza kutuletea walimu kupunguza upungufu huo kwa sasa? (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, kwanza katika utaratibu wa ajira za walimu lakini pia watumishi wa Sekta ya Afya kuanzia mwaka wa fedha 2021/2022 walimu na watumishi wa afya wanaomba kwa njia ya kielektroniki lakini wanapangiwa kwa uwiano na idadi kubwa kwenda kwenye halmashauri za pembezoni zenye upungufu mkubwa zaidi wa watumishi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali tayari imeshaanza kulifanyia kazi jambo hilo na ajira zote ambazo zitaendelea kuja zitakuwa zinakwenda kupeleka watumishi wengi zaidi maeneo ya vijijini na maeneo yenye upungufu mkubwa zaidi na Ofisi ya Rais, TAMISEMI tayari ina data base ya maeneo yote yenye changamoto kubwa zaidi ya walimu kama ilivyo Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nimhakikishie kwamba eneo hili la walimu tutaendelea kutoa kipaumbele katika Halmashauri hii ya Namtumbo na halmashauri nyingine zote za pembezoni likiwemo suala la upungufu wa walimu 418 ambalo kadiri ya ajira tutahakikisha kwamba tunatoa kipaumbele kupunguza gap ya watumishi katika Halmashauri ya Namtumbo, ahsante. (Makofi)

Name

Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. VITA R. KAWAWA aliuliza:- Je, lini Serikali itapeleka Walimu kukidhi mahitaji katika Shule za Sekondari na Msingi Wilayani Namtumbo?

Supplementary Question 2

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru; kutokana na upungufu wa walimu kuna walimu ambao wameendelea kujitolea katika shule za msingi na shule za sekondari kwa kulipwa na wananchi. Sasa ni kwa nini Serikali walau isiwape mkataba wa muda ili kuwapa motisha waendelee kufundisha wakati wakisubiri kuajiri walimu? (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana, Serikali ilikwishatoa kwanza maelekezo kwa Wakuu wa Shule lakini kwa maana ya Wakurugenzi katika Mamlaka ya Serikali za Mitaa kwamba wanaweza wakaajiri walimu wa kujitolea kwa muda wakati Serikali inaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya kuwaingiza kwenye utaratibu wa ajira za kudumu; kwa hiyo, jambo hilo linaendelea kufanyika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, namna ya kuweka mikataba, Serikali imeandaa mwongozo mahususi ambao utapelekea kuandaa mfumo ambao utawezesha walimu wanaojitolea kutambuliwa rasmi kwenye mfumo kuepuka udanganyifu wa baadhi ya Wakuu wa Shule wasiowaaminifu ambao mara nyingi wamekuwa wanaleta majina kwa mfano wakati wa ajira walimu ambao wanajitolea lakini wanaleta pia walimu ambao hawajitolei. Kwa hiyo, tunataka tuwe na mfumo mahususi ambao walimu wenyewe watajisajili na Ofisi ya Rais, TAMISEMI itakwenda kuhakiki na kujiridhisha ili ajira zinapotokea waweze kupata kipaumbele cha kuajiriwa katika ajira za kudumu, ahsante.

Name

Gibson Blasius Meiseyeki

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Arumeru-Magharibi

Primary Question

MHE. VITA R. KAWAWA aliuliza:- Je, lini Serikali itapeleka Walimu kukidhi mahitaji katika Shule za Sekondari na Msingi Wilayani Namtumbo?

Supplementary Question 3

MHE. ESTHER L. MIDIMU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali la nyongeza. Shule za Sekondari na Msingi Mkoa wa Simiyu zina upungufu mkubwa wa walimu. Je, ni lini Serikali itapeleka walimu wa kutosha katika shule za msingi na sekondari Mkoa wa Simiyu? (Makofi)

Name

Gibson Blasius Meiseyeki

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Arumeru-Magharibi

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, Serikali imeendelea kupeleka walimu wa Shule za Msingi na Sekondari katika Halmashauri zote za Mkoa wa Simiyu kuanzia ajira za 2021/2022, 2022/2023 lakini pia katika ajira za mwaka huu wa fedha 2023/2024 tutatoa kipaumbele kuhakikisha kwamba walimu zaidi wanaendelea kupelekwa katika shule za Mkoa wa Simiyu, ahsante.

Name

Sophia Hebron Mwakagenda

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. VITA R. KAWAWA aliuliza:- Je, lini Serikali itapeleka Walimu kukidhi mahitaji katika Shule za Sekondari na Msingi Wilayani Namtumbo?

Supplementary Question 4

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa swali la nyongeza. Mheshimiwa Waziri katika Bunge la Bajeti tulikuuliza swali la mfumo kuwakataa walimu wanaojitolea. Unaweza ukatoa ni lini Serikali itafanya haraka ili mfumo huo uweze kuwaelewa walimu wanaojitolea na waweze kupata ajira na kuachwa wakati muda mrefu wanajitolea?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kama alivyosema Mheshimiwa Mbunge kwamba wapo walimu ambao wamekuwa wakijitolea lakini mfumo wetu wa kuwatambua rasmi na kuthibitisha kwamba wanajitolea ili wapate kipaumbele cha ajira ulikuwa haujaandaliwa. Kwa hiyo, hivi sasa Serikali iko kwenye hatua za mwisho za kukamilisha mfumo ambao utawatambua na kuhakikisha kwamba wanaajiriwa kwa kipaumbele kila fursa zinapojitokeza, ahsante. (Makofi)