Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 13 Sitting 4 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 49 2023-11-03

Name

George Ranwell Mwenisongole

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbozi

Primary Question

MHE. GEORGE R. MWENISONGOLE aliuliza: -

Je, kwa nini wakulima wa kahawa Mbozi wanakatwa shilingi 200 kwa kilo licha ya tamko la kusitisha tozo hiyo?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, kwa niaba ya Waziri wa Kilimo naomba kujibu swali la Mheshimiwa George Ranwell Mwenisongole, Mbunge wa Jimbo la Mbozi kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inatekeleza Mkakati wa Maendeleo ya Tasnia ya Kahawa unaolenga kuongeza uzalishaji wa kahawa kutoka wastani wa tani 68,147 kwa mwaka wa fedha 2018/2019 hadi kufikia wastani wa tani 300,000 kwa mwaka wa fedha 2025/2026. Wadau wa kahawa walikubaliana kukusanya shilingi 200 kwa kilo ya kahawa safi ili kugharamia shughuli mbalimbali za maendeleo ya zao la kahawa kama zilivyoainishwa kwenye mkakati huo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, fedha hizo zinazokusanywa na Bodi ya Kahawa Tanzania zinatumika kutekeleza shughuli za maendeleo ya zao hilo zikiwemo uzalishaji wa miche bora, kuboresha shughuli za utafiti wa kahawa, upatikanaji wa pembejeo na kuimarisha masoko ya kahawa.