Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 14 Sitting 11 Public Service Management Ofisi ya Rais (Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora) 176 2024-02-13

Name

Santiel Eric Kirumba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SANTIEL E. KIRUMBA aliuliza: -

Je, Serikali haioni haja ya kuwapa Likizo ya uzazi zaidi ya siku 120 wanaojifungua watoto njiti ili kuwa na muda wa kutosha kuwatunza watoto hao?

Name

Ridhiwani Jakaya Kikwete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chalinze

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba sasa tuwatendee haki Wananchi wa Shinyanga waliyomchagua Mbunge Santiel Eric Kirumba, kwa kujibu swali Na. 176 kama lilivyoelekezwa kwenye Wizara yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, naomba kujibu swali Na. 176 lililoulizwa na Mheshimiwa Santiel Eric Kirumba, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Utumishi wa Umma, likizo ni miongoni mwa haki za watumishi wa umma ambazo wanastahili kupewa na waajiri wao kwa mujibu wa Kanuni H.12 ya Kanuni za Kudumu katika Utumishi wa Umma mwaka 2009, kanuni hiyo ikisomwa pamoja na Kanuni ya 97 ya Kanuni ya Utumishi wa Umma ya mwaka 2022.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la likizo ya mtumishi aliyejifungua mtoto njiti halijaelezwa bayana katika Kanuni za Kudumu za Utumishi wa Umma. Hata hivyo, kwa mujibu wa Kanuni ya 135 ya Kanuni ya Utumishi wa Umma ya mwaka 2022, linapotokea suala ambalo halikuelezwa bayana katika Kanuni ya Utumishi wa Umma, mtumishi atamtaarifu mwajiri kuhusu suala hilo. Mwajiri anaweza kutumia busara kulitatua pale inapobidi na anaweza kutumia sheria nyingine au kushauriana na Katibu Mkuu Utumishi kwa ufafanuzi wa suala hilo ikiwemo nyongeza ya siku katika likizo.