Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Santiel Eric Kirumba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SANTIEL E. KIRUMBA aliuliza: - Je, Serikali haioni haja ya kuwapa Likizo ya uzazi zaidi ya siku 120 wanaojifungua watoto njiti ili kuwa na muda wa kutosha kuwatunza watoto hao?

Supplementary Question 1

MHE. SANTIEL E. KIRUMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kutokana na majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri, amesema inategemea na busara; je, haoni kwamba Serikali inahitajika kuweka mkazo kwenye suala hili, kwa sababu siku 90 zile mama hazimtoshi kwa kipindi kile anapomlea mtoto njiti? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili. Je, Serikali pia haioni haja ya kuweka mkazo kwa wanaume pia kuwasaidia wanawake kwa kuwaongezea likizo ya uzazi wanaume wanaopata watoto njiti? (Makofi)

Name

Ridhiwani Jakaya Kikwete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chalinze

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza kuhusu kuweka utaratibu, nataka nilihakikishie Bunge lako kwamba maelekezo ya Bunge lako yalishatoka, lakini pia ni nia ya Mheshimiwa Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan ambaye alituelekeza sisi aliotupa dhamana ya kusimamia Ofisi ya Rais, Utumishi, kuyaangalia mazingira yote yatakayomwezesha mtumishi wa Umma kufanya kazi yake akiwa yupo na furaha ya kutimiza hayo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kufanya hivyo, Serikali imeandaa mwongozo wa ujumuishwaji wa jinsia katika Utumishi wa Umma mwaka 2023 ambao pamoja na masuala mengineyo tunazungumzia jambo la kutoa likizo kwa wazazi wanaopata watoto njiti likiwemo pia jambo hili la kuingiza wanaume katika sehemu ya watu watakaochukua likizo katika kipindi hicho cha kusaidiana kulea.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na hilo Serikali italeta mwongozo huu mbele ya Bunge lako, tutajadili kwa pamoja na tukubaliane kimsingi ni njia gani nzuri au ni kipindi gani kizuri cha kuwawekea wazazi hawa ili tuweze kufikia ulezi ulio bora usiochosha kwa mzazi mmoja au kwa mzazi mwingine, ahsante. (Makofi)