Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 13 Sitting 4 Water and Irrigation Wizara ya Maji 62 2023-11-03

Name

Vincent Paul Mbogo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkasi Kusini

Primary Question

MHE. VINCENT P. MBOGO aliuliza: -

Je, lini Serikali itapeleka mradi wa maji katika Kata za Kizumbi na Wampembe – Nkasi Kusini ?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri ya Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Vincent Paul Mbogo, Mbunge wa Jimbo la Nkasi Kusini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali katika mwaka wa fedha 2022/2023, imekamilisha usanifu wa Mradi wa Maji Wampembe utakaohudumia Kata mbili za Kizumbi na Wampembe. Utekelezaji wa mradi huo unatarajiwa kuanza mwezi Januari, 2024 na kukamilika mwezi Desemba, 2024 ambapo utanufaisha wananchi wapatao 15,089 waishio kwenye vijiji sita vya Wampembe, Mwinzana, Kizumbi, Lyapinda, Ng’anga na Katenge.

Mheshimwa Mwenyekiti, mradi huo unatarajiwa kutekelezwa na Serikali kwa kushirikiana na Shirika lisilo la Kiserikali la USAID kupitia Mradi wa Programu ya Maji na Usafi wa Mazingira (MUM), ambapo baadhi ya miundombinu inayotarajiwa kujengwa ni pamoja na matenki Manne (4) ya kuhifadhia maji yenye jumla ya lita 405,000, ujenzi wa vituo 39 vya kutolea huduma kwa wananchi sambamba na mtandao wa bomba kuu na mabomba ya usambazaji umbali wa Kilometa 41.