Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Vincent Paul Mbogo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkasi Kusini

Primary Question

MHE. VINCENT P. MBOGO aliuliza: - Je, lini Serikali itapeleka mradi wa maji katika Kata za Kizumbi na Wampembe – Nkasi Kusini ?

Supplementary Question 1

MHE. VINCENT P. MBOGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi kuweza kuuliza swali nyonyeza, nina maswali mawili.

Makao Makuu ya Wilaya ya Nkasi yana changamoto kubwa sana ya maji, ni nini mpango wa kutoa maji Ziwa Tanganyika ambao unaanzia Kata ya Wampembe kupeleka maji Wilayani Nkasi ?

Swali la Pili, Vijiji vya Mwinza, Diela, Katenge, Lupata, Lyapinda, Kasanga Ndogo, Katenge, Msamba, wananchi wanaliwa na Mamba wanapofuata huduma ya maji. Je, ni lini kama Wizara mtakaa na Wizara ya Maliasili ili muainishe maeneno yale ambayo wananchi wanapata huduma ya maji muwawekee wavu ili wananchi wasiliendelee kuliwa na mamba? Kwani ndani ya mwaka mmoja wameliwa watu Kumi. Ahsante sana. (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Maji, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, matumizi ya Ziwa Tanganyika kupeleka maji Makao Makuu ya Wilaya. Kwanza nampongeza Mheshimiwa Mbunge, umefuatilia sana na tayari Wizara tunaendelea na taratibu za kuona kwamba Ziwa Tanganyika tunaweza kuleta maji pale na maji yawe ya uhakika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la wananchi kuliwa na mamba. Mheshimiwa Mbunge nakupa pole sana kwa wananchi kupata hii kadhia, tutalichukulia kwa umakini mkubwa kuhakikisha kwamba tunakutana na wenzetu wa Maliasili basi tuje tuweke hiyo mipaka ya kuhakikisha wananchi wanachota maji maeneo yenye usalama. (Makofi)