Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 13 Sitting 4 Foreign Affairs and International Cooperation Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki 64 2023-11-03

Name

Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Primary Question

MHE. COSATO D. CHUMI aliuliza:-

Je, Taifa linanufaika kiasi gani katika uuzaji wa bidhaa na huduma katika maeneo ambayo Jeshi letu linafanya ulinzi wa amani?

Name

Amber. Mbarouk Nassor Mbarouk

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA AFRIKA MASHARIKI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Cosato David Chumi, Mbunge wa Mafinga Mjini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Tanzania imekuwa mstari wa mbele kushiriki katika jitihada mbalimbali za kutafuta amani kama ilivyoainishwa katika Sera ya Mambo ya Nje ya mwaka 2001. Hivyo, ushiriki wa Tanzania katika Misheni za Ulinzi wa Amani umekuwa na manufaa mbalimbali ikiwemo walinda amani wetu kufaidika na mafunzo ya ziada ambayo yanawajenga na kuwaimarisha; pia ajira za kiraia kwa Watanzania na kudumisha utamaduni wetu kupitia kukua kwa lugha ya Kiswahili, kwani katika maeneo mengi ya DRC, Lebanon na Darfur, kumekuwa na ongezeko la matumizi ya Kiswahili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na manufaa yaliyoainishwa, zipo fursa za kiuchumi zinazopatikana katika shughuli za ulinzi wa amani, ikiwa ni pamoja na biashara ya bidhaa zinazoweza kutumika katika vikosi vilivyopo katika misheni hizo, kama vile chakula, mavazi, vinywaji, vifaa tiba na madawa. Fursa nyingine ni usafirishaji wa mizigo, ujenzi wa majengo yanayohamishika, vifaa, huduma za TEHAMA na nyinginezo. Aidha, Tanzania inaweza pia kuuza teknolojia ya kutumia panya katika kubaini na kutegua mabomu ambayo yametegwa ardhini kama fursa za kiuchumi, ahsante sana.