Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Primary Question

MHE. COSATO D. CHUMI aliuliza:- Je, Taifa linanufaika kiasi gani katika uuzaji wa bidhaa na huduma katika maeneo ambayo Jeshi letu linafanya ulinzi wa amani?

Supplementary Question 1

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi na kwa majibu mazuri ya Serikali. Nitakuwa na swali moja la nyongeza. Kabla ya swali hilo napenda kutumia nafasi hii kuipongeza nchi yetu ya Tanzania kwa kuendelea kuwa kinara katika masuala ya ulinzi wa amani kama ambavyo tulikuwa kinara katika ukombozi wa Kusini Barani Afrika. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu ni moja; kwa sababu kuna hizo fursa, je, Wizara ipo tayari kuwa Wizara kiongozi kwa kushirikiana na Wizara ya Viwanda na Biashara ili kuendelea kung’amua fursa hizo kwa kushirikiana labda na NBC pamoja na TPSF kufanya kongamano ambalo linaweza likawasaidia wafanyabiashara wa Tanzania kung’amua hizo fursa na hivyo kunufaika kiuchumi kama Taifa?

Name

Amber. Mbarouk Nassor Mbarouk

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA AFRIKA MASHARIKI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. Serikali inatambua umuhimu wa kuwania fursa ambazo zinapatikana katika uendeshaji wa operesheni za ulinzi wa amani. Kwa kutambua hilo, mwezi Januari mwaka huu, 2023, Serikali iliandaa semina mahususi kwa wafanyabiashara kuhusiana na fursa zilizopo katika maeneo ya operesheni hizo. Lengo hasa la semina hiyo ilikuwa ni kuwapa elimu na kuwahamasisha wafanyabiashara wa Tanzania juu ya fursa mbalimbali ambazo zipo katika Operesheni za Ulinzi wa Amani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kulifahamisha Bunge lako Tukufu kwamba matunda ya semina hiyo tayari yameanza kuonekana, kwani hivi sasa wafanyabiashara wengi wa Tanzania wanachangamkia fursa hizo ambazo zipo katika Pperesheni za Ulinzi wa Amani katika sehemu mbalimbali, nakushukuru sana.