Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 13 Sitting 4 Defence and National Service Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga taifa 66 2023-11-03

Name

Justin Lazaro Nyamoga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilolo

Primary Question

MHE. JUSTIN L. NYAMOGA aliuliza:-

Je, lini Jeshi la Wananchi litatimiza ahadi yake ya kujenga daraja la dharura katika Mto Mtitu Kata ya Ihimbo?

Name

Dr. Stergomena Lawrence Tax

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI K.n.y. WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA aljibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa napenda kujibu swali la Mheshimiwa Justin Lazaro Nyamoga, Mbunge wa Kilolo, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, majukumu ya kuendeleza na kusimamia barabara za vijijini na mijini ambayo awali yalikuwa yakitekelezwa na Mamlaka za Serikali za Mitaa yamekabidhiwa kwa Wakala wa Barabara za Vijijini Tanzania (TARURA). Hata hivyo, mwezi Julai, 2022 Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa ilipokea maombi ya kujengewa daraja la dharura katika Mto Mtitu, Kata ya Ihimbo kutoka Ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Kilolo Mkoani Iringa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara kupitia Jeshi la Wananchi wa Tanzania ilipeleka kikundi cha Wahandisi wa Medani ambacho kilifanya uchambuzi wa madaraja ya chuma yaliyopo na kubaini kuwa lipo daraja la JWTZ la Bailey Bridge lililopo yadi za TARURA mkoani Mbeya ambalo lingefaa kujengwa katika eneo husika. Aidha, Halmashauri ya Wilaya ya Kilolo inashauriwa kukamilisha ujenzi wa barabara ya vumbi yenye uwezo wa kupitisha magari ya tani 20 pamoja na uimarishaji wa eneo jipya la ujenzi wa daraja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ili kutatua changamoto ya kukosekana kwa mawasiliano baina ya wananchi wa Kata ya Ihimbo na maeneo mengine, Wizara inapendekeza kukutana na Mheshimiwa Mbunge pamoja na Ofisi ya TARURA Wilaya ya Kilolo ili kutatua changamoto hiyo.