Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Justin Lazaro Nyamoga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilolo

Primary Question

MHE. JUSTIN L. NYAMOGA aliuliza:- Je, lini Jeshi la Wananchi litatimiza ahadi yake ya kujenga daraja la dharura katika Mto Mtitu Kata ya Ihimbo?

Supplementary Question 1

MHE. JUSTIN L. NYAMOGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa majibu mazuri ya Serikali. Sasa nina maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza, kwa kuwa tayari daraja lipo kule Mbeya; na kwa kuwa Wizara tayari ilishabaini mahitaji kwamba kuna mahitaji ya daraja hilo.

Je, ni lini tutafanya hicho kikao na Wizara ya Ulinzi kwa sababu sisi Kilolo tuko tayari ili utekelezaji uanze kufanyika? Hilo ni swali la kwanza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; je, Serikali haioni umuhimu wa kufanya haraka kwa sababu kipindi cha msimu wa mvua ambacho ndiyo huwa kina matatizo makubwa kimekaribia na ikiwa tutachelewa, madhara makubwa yanaweza kutokea, kwa sababu kila mwaka tunapoteza watu kama hatutaweza kujenga hilo daraja?

Name

January Yusuf Makamba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bumbuli

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI K.n.y. WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Nyamoga, Mbunge wa Kilolo, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nikubaliane na Mheshimiwa Mbunge juu ya umuhimu na uharaka wa ujenzi wa daraja hili, lakini nampongeza pia kwa utayari wake. Kama nilivyomjibu katika swali la msingi kwamba Wizara iko tayari kukutana naye pamoja na TARURA, hivyo, namwomba Mheshimiwa Mbunge baada ya kikao hiki niweze kukutananaye na pale ambapo atakuja Mheshimiwa Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, nimfikishie ujumbe huu waweze kufanya kikao hicho kwa haraka na suala hilo liweze kupatiwa ufumbuzi.