Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 13 Sitting 6 Health and Social Welfare Wizara ya Afya 78 2023-11-06

Name

Zainab Athuman Katimba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. KILUMBE S. NG’ENDA K.n.y. MHE. ZAINAB A. KATIMBA aliuliza: -

Je, lini Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Magharibi itaanza kujengwa?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Afya naomba kujibu swali la Mheshimiwa Zainab Athman Katimba, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2023/2024 Serikali imetenga kiasi cha shilingi bilioni tano kwa ajili ya kuanza Ujenzi wa Hospitali ya Kanda ya Magharibi ambapo ujenzi utaanza na jengo la huduma za wagonjwa wa nje (OPD).

Mheshimiwa Spika, ujenzi huu utaanza mwezi Januari 2024, ahsante.