Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 13 Sitting 4 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Waziri wa Mifugo na Uvuvi 67 2023-11-03

Name

Yustina Arcadius Rahhi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. YUSTINA A. RAHHI aliuliza:-

Je, Serikali ina mpango gani wa utambuzi wa mifugo baada ya kusitisha zoezi la utambuzi kwa kutumia hereni za mifugo?

MWENYEKITI: Mheshimiwa Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mheshimiwa Alexander Mnyeti majibu.

Name

Alexander Pastory Mnyeti

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Misungwi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Mifugo na Uvuvi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Yustina Arcadius Rahhi, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwezi Novemba, 2022 Serikali ilisitisha kwa muda zoezi la utambuzi wa mifugo kwa njia ya hereni ili kurekebisha kasoro zilizojitokeza ambazo ni pamoja na wafugaji kulalamika juu ya bei ya kuvisha hereni na baadhi ya wafugaji kukosa elimu sahihi ya utambuzi wa mifugo hiyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara imekamilisha kufanya marekebisho ya kasoro la zoezi hilo la utambuzi zilizojitokeza ambapo bei ya kuvika hereni imeshuka kutoka 1,750 hadi shilingi 1,550 kwa ng’ombe na kutoka shilingi 1,000 kwa mbuzi na kondoo hadi shilingi 900. Pia, Wizara imekamilisha kuandaa mkakati wa utoaji elimu kwa wafugaji kuhusu umuhimu wa utambuzi wa mifugo hiyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mwaka wa fedha 2023/2024 Wizara kwa kushirikiana na wadau wa mifugo, inategemea kuanza awamu ya pili ya utambuzi wa mifugo kwa kuanza na mashamba makubwa ya mifugo ya Serikali, mashirika, watu binafsi, wawekezaji kwenye vitalu vya NARCO, vituo vya unenepeshaji ng’ombe wa maziwa, wafugaji wakubwa na wafugaji watakaokuwa tayari wakati wa zoezi hilo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha.