Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 13 Sitting 6 Water and Irrigation Wizara ya Maji 79 2023-11-06

Name

Daimu Iddi Mpakate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kusini

Primary Question

MHE. DAIMU I. MPAKATE aliuliza: -

Je, lini wananchi wa Kata za Nalasi Tunduru watapata maji ya uhakika?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu,

Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Maji naomba kujibu swali la Mheshimiwa Daimu Iddi Mpakate, Mbunge wa Jimbo la Tunduru Kusini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Kata mbili za Nalasi Mashariki na Nalasi Magharibi zenye jumla ya ya wakazi 21,989; na vijiji saba vya Nalasi, Wenje, Lipepo, Mkapunda, Lukumbo, Nasomba na Chilundundu zinapata huduma ya maji kupitia Skimu ya Maji ya Nalasi na Nasomba zilizojengwa mwaka 2012. Katika kuboresha huduma ya maji kwenye kata hizo, Serikali katika mwaka wa fedha 2023/2024 itafanya ukarabati wa miradi hiyo ili kuongeza ufanisi wa utoaji huduma ambapo utekelezaji wake unatarajiwa kuanza mwishoni mwa mwezi Novemba, 2023 na kukamilika Februari, 2024.

Mheshimiwa Spika, Serikali pia katika mwaka huu wa sedha 2023/2024, itafanya utafiti wa maji chini ya ardhi pamoja na kuchimba visima virefu vya maji katika Vijiji vya Nalasi, Wenje na Mkapunda ili kupata vyanzo vya uhakika vitakavyosaidia kujenga mradi mkubwa wa usambazaji maji utakaoweza kuhudumia vijiji vyote vya Kata zote mbili za Nalasi Mashariki na Nalasi Magharibi. Kazi ya utafiti wa uchimbaji visima hivyo, inatarajiwa kuanza mwishoni mwa mwezi Novemba, 2023 na kukamilika Februari, 2024.