Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Daimu Iddi Mpakate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kusini

Primary Question

MHE. DAIMU I. MPAKATE aliuliza: - Je, lini wananchi wa Kata za Nalasi Tunduru watapata maji ya uhakika?

Supplementary Question 1

MHE. DAIMU I. MPAKATE: Mheshimiwa Spika, ahsante. Skimu ya Nalasi iligharimu zaidi ya milioni 800 na ilifanya kazi kwa mwezi mmoja, na sasa haifanyi kazi kutokana na matatizo ya kiufundi. Katika kampeni tuliahidi kwamba Skimu hiyo itafanyiwa matengenezo, lakini mpaka sasa hii ni mara ya pili nauliza swali hili naambiwa litafanyiwa maboresho;

Je, ni lini Serikali itafanya maboresho makubwa kwenye skimu ile ambayo imegharimu pesa nyingi na haifanyi kazi, ili wananchi wa Vijiji vya Nalasi, Lipepo na Chilundundu vipate huduma ya maji?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; mwaka jana mwezi Agosti RUWASA Mkoa waliingia makataba na Kampuni ya Chikwale Company Limited wa uchimbaji visima 18, pamoja na kisima kimoja kirefu katika Kijiji cha Nalasi na Vijiji vingine vya Azimio, Semeni, Angalia na Mwenge ili kuboresha upatikanaji wa maji, lakini mkandarasi yule mpka sasa hajafanya kazi ya aina yoyote;

Je, ni lini Serikali itapeleka Mkandarasi mwingine mwenye uwezo wakuchimba visima vile ili kuwapatia maji wananchi wa Jimbo la Tunduru Kusini? (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Daimu Mpakate, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kuhusu swali linalosema ni lini tutafanya ukarabati wa Skimu hii ya Nalasi; kama nilivyiojibu kwenye jibu langu la msingi; Mheshimiwa Mbunge naomba uamini kwamba sisi tutakuja kukamilisha ukarabati huu kadiri ya muda huu tulioahidi hapa na nitasimamia. Mheshimiwa Mbunge tutafika pamoja katika mradi huu na kuhakikisha unafanyiwa kazi.

Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali namba mbili, kwamba ni lini Mkandarasi mwingine apatiwe aweze kuchimba visima hivi; naomba niwe nimelichukua tukalifanyie mchakato kuona kwa nini huyu ameshindwa na kuona namna njema ya kuhakikisha visima hivyo vinachimbwa.

Name

Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Primary Question

MHE. DAIMU I. MPAKATE aliuliza: - Je, lini wananchi wa Kata za Nalasi Tunduru watapata maji ya uhakika?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. ANGELINE S. L. MABULA: Mheshimiwa Spika, naomba kumuuliza Naibu Waziri, kwanza kwa kuwashukuru namna ambavyo wanatatua kero ya maji katika Jiji la Mwanza hususani Wilaya ya Ilemela. Wamekuja na mkakati wa matokeo ya muda mfupi, wameanza kusambaza sim tank katika maeneo yenye changamoto.

SPIKA: Swali Mheshimiwa, mmesimama Wabunge wengi.

MHE. DKT. ANGELINE S. L. MABULA: Mheshimiwa Spika, swali langu ni kwamba walishafanya survey katika maeneo ambyo wanaweza kuchimba visima kwa ajili ya ku-save maji hapo;

Je, ni lini visima vitajengwa katika Kata ya Kayenze Mtaa wa Lutongo ambako tayari feasibility study imeshafanyika na maji yalipatikana?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Angeline Mabula kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli tumeshafanya survey na baadhi ya maeneo katika vijiji hivyo alivyovitaja tumepata maji. Katika eneo la kata aliyoitaja tumepata maji kidogo lakini maji hayo tutahakikisha tutayatumia kujenga vichotea maji vichache ili wananchi wale waweze kupata huduma ya maji.

Name

Catherine Valentine Magige

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DAIMU I. MPAKATE aliuliza: - Je, lini wananchi wa Kata za Nalasi Tunduru watapata maji ya uhakika?

Supplementary Question 3

MHE. CATHERINE V. MAGIGE: Mheshimiwa Spika, je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi yake ya Mradi wa Maji katika Wilaya ya Monduli ambao utapita katika Vijiji vya Mbuyuni, Makuyuni, Losimingoli na Naiti? (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Nomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Catherine Magige kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwa eneo la Monduli kazi mbalimbali zinaendelea kwenye mradi huu na niseme katika mwaka huu wa sedha, tutahakikisha tunakamilisha wananchi waweze kupata maji safi na salama.

Name

Hussein Nassor Amar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyang'hwale

Primary Question

MHE. DAIMU I. MPAKATE aliuliza: - Je, lini wananchi wa Kata za Nalasi Tunduru watapata maji ya uhakika?

Supplementary Question 4

MHE. HUSSEIN N. AMAR: Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwa kuwa wananchi wengi Wilaya ya Nyang’wale wamefungiwa mita za maji na kushindwa kuendelea kutumia maji yale kwa ajili ya mita zao kwenda speed sana na kuwa bili kubwa;

Je, Serikali ipo tayari kutuma tume kwenda kuchunguza mita hizo?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Hussein Amar, Mbunge wa Nyang’wale kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, tutatuma wataalam waweze kwenda kuchunguza mita hizo ili wananchi waweze kulipia bili kulingana na matumizi yao.

Name

Daniel Baran Sillo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Babati Vijijini

Primary Question

MHE. DAIMU I. MPAKATE aliuliza: - Je, lini wananchi wa Kata za Nalasi Tunduru watapata maji ya uhakika?

Supplementary Question 5

MHE. DANIEL B. SILLO: Mheshimiwa Spika, ahsante. Mkataba kwa ajili ya ujenzi wa maji wa Ziwa Madunga ulitakiwa usainiwe tangu 15 Oktoba, lakini mpaka leo haujasainiwa;

Je, ni lini mkataba huu utasainiwa ili wananchi wapate maji safi na salama?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Sillo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, mradi huu wa Ziwa Madunga tunatarajia wiki hii Mheshimiwa Mbunge, kama ambavyo tumeweza kuwasiliana ofisini, tutahakikisha mkataba huu unasainiwa.