Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 13 Sitting 6 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 82 2023-11-06

Name

Stanslaus Haroon Nyongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Mashariki

Primary Question

MHE. STANSALAUS H. NYONGO aliuliza: -

Je, lini jengo la Mahabusu katika Gereza la Maswa litakarabatiwa?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu,

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Stanslaus Haroon Nyongo, Mbunge wa Maswa Mashariki kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Gereza la Maswa ni miongoni mwa magereza makongwe yaliyojengwa tangu kipindi cha ukoloni ambapo miundombinu yake inahitaji ukarabati.

Mheshimiwa Spika, katika kukabiliana na changamoto hiyo, Serikali kupitia Jeshi la Magereza inaendelea kuyafanyia ukarabati mdogo magereza nchini likiwemo Gereza la Maswa kwa kutumia fedha zinazotokana na vyanzo vya ndani. Gereza la Maswa limepangwa kuanza kufanyiwa ukarabati katika mwaka huu wa fedha 2023/2024, ahsante.