Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Stanslaus Haroon Nyongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Mashariki

Primary Question

MHE. STANSALAUS H. NYONGO aliuliza: - Je, lini jengo la Mahabusu katika Gereza la Maswa litakarabatiwa?

Supplementary Question 1

MHE. STANSALAUS H. NYONGO: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kwa majibu mazuri ya Serikali. Gereza la Maswa kama majibu ya Serikali yanavyosema ni Gereza kongwe la siku nyingi na ukarabati inawezekana ukatumia gharama kubwa, na Magereza hii ipo katikati Maswa Mjini;

Je, Serikali ipo tayari tuwapatie kiwanja nje ya mji na lile gereza mkabadilisha ikiwezekana na magereza mengine, yale magereza ya mjini mkayafanya kuwa business complex mkapata vyanzo zaidi vya ndani?

Je, mna mpango gani na zile nyumba za wafanyakazi pale Maswa ambazo nazo nazo zina hali mbaya?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, nikiri, kama alivyosema Mheshimiwa Mbunge kwamba, Magereza ya mjini hasa ile ya Maswa ni kongwe na limechakaa sana. Nikubaliane na yeye tu baada ya Bunge hili ninatarajia kufanya ziara Mkoani Simiyu.

Pamoja na mambo mengine nitatembelea eneo la Maswa. Kama atakuwa na nafasi tukaenda wote tuone namna ambavyo tunaweza tukalifanyia ukarabati Gereza hili au kukubaliana mpango wake wa kupata eneo jingine la kujenga magereza.

Mheshimiwa Spika, kuhusu nyumba tunavyofanya ukarabati wa magereza ni pamoja na majengo yenyewe ya magereza, kwa maana ya mahabusu na vyumba wanavyokaa wafungwa, pamoja na nyumba za watumishi wakiwemo askari. Kwa hiyo, tutakapofanya ukarabati maeneo yote mawili yatazingatiwa, nashukuru.