Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 14 Sitting 11 Finance Wizara ya Fedha 188 2024-02-13

Name

Angelina Adam Malembeka

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ANGELINA ADAM MALEMBEKA aliuliza: -

Je, lini Serikali itabadili muonekano wa Noti na Sarafu ili kutoa fursa ya kuweka picha ya Rais Mwanamke wa kwanza Tanzania?

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, uamuzi wa kuondoa picha ya Rais kwenye noti ulifanyika katika kipindi cha Awamu ya Tatu chini ya Rais mstaafu Hayati Benjamin Mkapa. Miongoni mwa sababu ya kuondoa picha za viongozi kwenye sarafu yetu ilikuwa ni gharama za mara kwa mara za uchapishaji wa noti kwa ajili ya kubadilisha picha za viongozi mara muda wao wa kuwa madarakani unapokoma. Hivyo, kuanzia toleo la noti la mwaka 1997, picha ya Kiongozi Mkuu wa Nchi iliondolewa na badala yake picha za wanyama kama vile tembo (shilingi 10,000), kifaru (shilingi 5,000) na simba (shilingi 2,000) zimeendelea kuonekana kwenye sarafu ya nchi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kuenzi michango ya waasisi wa Taifa letu, noti ya shilingi 1,000 imeendelea kuchapishwa ikiwa na picha ya baba wa Taifa Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na noti ya shilingi 500 ilichapichwa ikiwa na picha ya Rais wa awamu ya kwanza wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Hayati Sheikh Abeid Amani Karume. Hata hivyo, noti ya shilingi 500 ilibadilishwa kuwa coin mwaka 2014 ambapo picha ya Hayati Sheikh Abeid Amani Karume imeendelea kuwepo. Ahsante. (Makofi)