Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Angelina Adam Malembeka

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ANGELINA ADAM MALEMBEKA aliuliza: - Je, lini Serikali itabadili muonekano wa Noti na Sarafu ili kutoa fursa ya kuweka picha ya Rais Mwanamke wa kwanza Tanzania?

Supplementary Question 1

MHE. ANGELINA ADAM MALEMBEKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali ya nyongeza. Kwanza, namshukuru Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu yake mazuri ambayo yametuwekea kumbukumbu kwamba, mara ya mwisho tulibadilisha fedha mwaka 1997 lakini jibu langu bado sijalipata. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa, ni mara ya kwanza kupata Rais Mwanamke Tanzania na Afrika Mashariki, ambaye ni mchapa kazi, jasiri na ameonyesha uwezo wa wanawake. Ambaye ameweza kutupa sifa Tanzania, Afrika na dunia nzima. Je, Serikali haioni kwamba, sasa ni wakati mwafaka wa kuweka sura ya Rais wa Kwanza Mwanamke katika Noti za Tanzania? (Makofi)

Swali langu la pili, kwa kuwa, Rais wa Kwanza wa Zanzibar amepewa nafasi katika sarafu ya Shilingi 500 na kutokana na kupanda kwa uchumi sasa hivi, Shilingi 500 haitumiki sana. Je, Serikali haioni kwamba sasa hivi ni fursa pekee ya kupandisha pia hadhi ya Rais wa Kwanza wa Zanzibar, kumuongezea noti juu? (Makofi)

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Angelina kwa pamoja kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu suala hili zipo taratibu mbalimbali ambazo hutumika katika uwekaji wa alama kwenye noti zetu au sarafu yetu. Hizi lazima zizingatie kufuata Taratibu, Sheria na Kanuni. Muda wa suala hili ukifika basi, maoni yake tumeyachukua na tunaenda kuyafanyia kazi. Muda ukifika zitawekwa, Inshallah. (Makofi)