Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 13 Sitting 10 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 135 2023-11-10

Name

Seif Khamis Said Gulamali

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manonga

Primary Question

MHE. TUNZA I. MALAPO K.n.y. MHE. SEIF K. S. GULAMALI aliuliza: -

Je, lini Serikali itaugawa Mkoa wa Tabora na kupata Mkoa mpya wa Manonga?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Seif Khamis Said Gulamali, Mbunge wa Jimbo la Manonga, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, mchakato wa kuanzisha eneo la Utawala la Mkoa unafanyika kwa mujibu wa sheria, kanuni na taratibu zilizopo baada ya Idhini/Kibali kutolewa na Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kwa kuzingatia Sheria inayohusu kuanzisha Mkoa na Wilaya, Sura Na. 397 na Mwongozo wa kuanzisha Maeneo Mapya ya Utawala wa mwaka 2014.

Mheshimiwa Spika, maombi ya kuanzishwa Mkoa mpya yanatakiwa kujadiliwa, kupitishwa na kuridhiwa kwenye vikao vya Kisheria ngazi ya Vijiji, Kata, Baraza la Madiwani, Kamati ya Ushauri ya Wilaya, Kamati ya Ushauri ya Mkoa kisha kuwasilishwa Ofisi ya Rais, TAMISEMI kwa ajili ya tathmini ya vigezo.

Mheshimiwa Spika, kutokana na uhitaji mkubwa wa miundombinu na rasilimali nyingine katika mikoa iliyopo, Serikali imeweka kipaumbele katika kuboresha na kukamilisha miundombinu msingi kwenye maeneo ya kiutawala yaliyopo ili yaweze kutoa huduma kwa ufanisi zaidi na baadaye kuendelea na maeneo mengine kwa kufuata taratibu na vigezo vilivyoainishwa, ahsante.