Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Tunza Issa Malapo

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TUNZA I. MALAPO K.n.y. MHE. SEIF K. S. GULAMALI aliuliza: - Je, lini Serikali itaugawa Mkoa wa Tabora na kupata Mkoa mpya wa Manonga?

Supplementary Question 1

MHE. TUNZA I. MALAPO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Nina swali moja la nyongeza, lengo la kugawa maeneo ya utawala ni kurahisisha huduma kwa wananchi, lakini hapa nchini kuna Majimbo mengi sana makubwa ikiwemo Jimbo la Mbeya Mjini, Tandahimba na sehemu nyingine; je, Serikali ina mkakati gani wa kuyagawa Majimbo hayo ili huduma kwa wananchi ziwe rahisi? Nakushukuru. (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Tunza Malapo, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba lengo la kugawa maeneo mapya ya utawala yakiwemo majimbo ni kusogeza huduma za kijamii karibu zaidi na wananchi na Serikali inatambua uhitaji wa maeneo haya. Kwa hivyo kwa utaratibu uliopo, kwa mujibu wa mwongozo lakini na sheria, mamlaka husika wanatakiwa kufuata utaratibu huo kwa maana ya Vikao Ngazi ya Vijiji, Baraza la Madiwani, DCC, RCC na kuwasilisha Ofisi ya Rais, TAMISEMI na pale ambapo Serikali itaona inafaa kugawa maeneo hayo ya utawala mapya basi taratibu zitafuata na maeneo hayo yatagawiwa katika utaratibu ulipo, ahsante.

Name

Mussa Ramadhani Sima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Mjini

Primary Question

MHE. TUNZA I. MALAPO K.n.y. MHE. SEIF K. S. GULAMALI aliuliza: - Je, lini Serikali itaugawa Mkoa wa Tabora na kupata Mkoa mpya wa Manonga?

Supplementary Question 2

MHE. MUSSA R. SIMA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru, kwa kuwa imefanyika sensa hapa hivi karibuni na ziko kata zimeonekana ni kubwa zaidi zinahitaji mgawanyo pamoja na tarafa ikiwemo Kata ya Mandewa na Kata ya Minga. Nataka kujua mkakati wa Serikali ni nini kifanyike sasa ili kuweza kuzigawa kata hizo na kusogeza huduma kwa wananchi?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana, naomba kujibu swali la nyongeza Mheshimiwa Mussa Sima, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kwanza tunafahamu kwamba kuna kata kubwa, kuna tarafa kubwa na Serikali inatambua inatambua umuhimu wa kugawa maeneo hayo kusogeza huduma za kijamii, lakini utaratibu ni uleule tuanze kwenye Vikao vya Kisheria katika ngazi zetu za Vijiji, Kata, Wilaya, Mkoa kisha kuwasilisha Ofisi ya Rais, TAMISEMI kwa ajili ya kufanya tathimini ya vigezo hivyo na kuona uwezekano wa kupata maeneo hayo, ahsante. (Makofi)

Name

Charles Muguta Kajege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mwibara

Primary Question

MHE. TUNZA I. MALAPO K.n.y. MHE. SEIF K. S. GULAMALI aliuliza: - Je, lini Serikali itaugawa Mkoa wa Tabora na kupata Mkoa mpya wa Manonga?

Supplementary Question 3

MHE. CHARLES M. KAJEGE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Ukiona mchakato uliopo sasa hivi kufikia uamuzi huo ni mrefu sana. Kwa nini Serikali isiachie jukumu hilo katika level ya juu (Serikali Kuu) ndiyo ifanye maamuzi badala ya vikao vyote hivyo?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana, utaratibu huu umewekwa kwa sababu kugawa maeneo ya kiutawala pia kuna hitaji ridhaa ya wananchi kutoka katika maeneo husika. Serikali hii sikivu Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan na Serikali ya Awamu ya Sita, lakini hata Serikali zilizopita zinahitaji kuwashirikisha wananchi katika kugawa maeneo yao ya utawala ndiyo maana mfumo huu ni muhimu na vizuri sana utaratibu huu ukafuatwa, ahsante. (Makofi)

Name

Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Primary Question

MHE. TUNZA I. MALAPO K.n.y. MHE. SEIF K. S. GULAMALI aliuliza: - Je, lini Serikali itaugawa Mkoa wa Tabora na kupata Mkoa mpya wa Manonga?

Supplementary Question 4

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi. Kama alivyosema Mheshimiwa Kajege Sensa ya Watu na Makazi mojawapo ya jambo la kutusaidia ni kupanga Mipango ya Maendeleo.

Je, Serikali haioni kwamba kwa kutumia Taarifa na Takwimu za Sensa ya Watu na Makazi ikaona kabisa kuna maeneo yanahitaji kufanya mgawanyo then yenyewe ikashusha kwetu sisi wananchi na sisi tukasema ndiyo au hapana?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Cosato David Mchumi, Mbunge wa Mafinga Mjini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, taratibu ambazo zimewekwa kwa mujibu wa sheria ni sheria ambazo sisi kama Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tulizitunga na lengo la sheria hizi kama nilivyotangulia kusema ni kuhakikisha kwamba tunawashirikisha wananchi katika kuamua mipaka, lakini pia kupata maeneo ya utawala.

Kwa hiyo nafikiri utaratibu huu ambao upo ni muhimu ufuatwe, lakini kama kuna maoni zaidi ya kuona ni namna gani tunaweza tukaboresha basi Serikali iko tayari kusikiliza maoni na kuyafanyia kazi, ahsante.