Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 13 Sitting 10 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 137 2023-11-10

Name

Santiel Eric Kirumba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SANTIEL E. KIRUMBA aliuliza:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kushirikiana na Sekta Binafsi ili kutoa chakula mashuleni?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Santiel Eric Kirumba, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali ina wadau mbalimbali wanaounga mkono jitihada za Serikali katika utoaji wa huduma ya chakula na lishe shuleni. Baadhi ya wadau hao ni kama vile Shirika la Mpango wa Chakula Duniani (WFP), United Nations Children's Fund (UNICEF), World Vision, Feed the Children, SANKU, GAIN Tanzania, Project Concern International (PCI), CiC, Save the Children.

Mheshimiwa Spika, wadau hao hufanya kazi kwa kushirikiana na Serikali katika kuzijengea uwezo Kamati za Shule namna ya ushirikishwaji wa wazazi/walezi katika upatikanaji wa chakula cha wanafunzi shuleni, kutoa elimu ya uongezaji wa virutubisho katika chakula cha wanafunzi shuleni (fortified foods); kuhamasisha upatikanaji wa matumizi ya mazao lishe (biofortified) yakiwemo maharage, mahindi ya njano, kwa ajili ya uji wa wanafunzi; kushirikiana na shule zenye utayari wa kuendesha shughuli za kilimo cha mazao ya chakula kwa kugawa mbegu za mahindi na maharage shuleni; na kuandaa miongozo ya utoaji wa huduma ya chakula na lishe shuleni.

Mheshimiwa Spika, mpango upo na unatekelezwa kwa kushirikisha wadau ili kuendelea na mpango wa kutoa chakula.