Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Santiel Eric Kirumba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SANTIEL E. KIRUMBA aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kushirikiana na Sekta Binafsi ili kutoa chakula mashuleni?

Supplementary Question 1

MHE. SANTIEL E. KIRUMBA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa majibu mazuri ya Serikali, licha ya hivyo nina maswali madogo mawili ya nyongeza.

Swali la kwanza; mradi huu umekuwa ukikabiliwa na changamoto ndogo ndogo ambazo ni ukosefu wa miundombinu, maji safi na salama, ongezeko la shule mpya nyingi ambazo haziko kwenye mradi, zimepelekea watoto wetu wanapokuwa shuleni kukosa chakula.

Mheshimiwa Spika, swali la pili; Wadau hawa wa Sekta ya Elimu wameelekeza watoto wanapokuwa shuleni wafundishwe namna bora ya kupanda mbogamboga na kupanda matunda ili yaweze kuwasaidia kupata mlo bora ambao utawatoa wasiweze kushindwa kupata udumavu, ahsante. (Makofi)

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, nikijibu maswali ya nyongeza ya Mheshimiwa Santiel Kirumba; la kwanza, hili la ukosefu wa miundombinu mbalimbali hasa katika shule mpya ambazo zimejengwa hivi karibuni miundombinu kama maji na kadhalika. Tunashirikiana na Wizara ya Maji, Wizara ya Nishati na kadhalika katika kuhakikisha miundombinu muhimu inafika katika Taasisi zetu za Serikali kwenye maeneo mbalimbali hapa nchini ikiwemo shule na tutaendelea kufanya hivyo ili kuhakikisha huduma bora inatolewa katika shule zetu zote hapa nchini.

Mheshimiwa Spika, nikienda kwenye swali lake la pili; Kuna club mbalimbali katika shule zetu katika kuhakikisha kwamba upandaji wa mbogamboga unafanyika na kuendelea kufundishwa kwa wanafunzi wetu katika shule zile na Serikali itaendelea kutilia mkazo uwepo wa club hizi. Hivyo basi, nitumie nafasi hii kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI kuwaelekeza ma-REO wote na ma-DEO wote nchini (Maafisa Elimu Mkoa na Maafisa Elimu Wilaya) kuhakikisha kwamba club hizi za upandaji wa mbogamboga zinaendelezwa katika shule zetu za sekondari na shule zetu za msingi nchini kote.