Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 13 Sitting 10 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 138 2023-11-10

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Primary Question

MHE. JAPHET N. HASUNGA aliuliza:-

Je, lini Serikali itatoa fedha kumalizia ujenzi wa maboma ya shule za msingi na sekondari yaliyojengwa kwa nguvu za wananchi Mbozi?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Japhet Ngailonga Hasunga, Mbunge wa Jimbo la Vwawa, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali ina utaratibu wa kukusanya takwimu za maboma yaliyojengwa na wananchi katika Mamlaka za Serikali za Mitaa ili kuweka mkakati na mpango wa ukamilishaji.

Mheshimiwa Spika, ni kweli Halmashauri ya Mbozi ina maboma mengi ya madarasa yaliyojengwa kwa nguvu za wananchi. Mwaka 2020/2021 kulikuwa na maboma 1,529 yakiwepo madarasa ya shule za msingi 1,513 na sekondari 86. Yaliyopo kwa sasa baada ya Serikali kwa kushirikiana na Wadau na wananchi kuyakamilisha ni ya shule za msingi 1,386 na sekondari 76 ambayo kati ya hayo 64 yamepauliwa. Aidha, maboma yaliyotengewa bajeti kwa kipindi cha 2023/2024 ni 18. Serikali kwa kushirikiana na wadau imeendelea kuyapunguza kadri inavyopata fedha.