Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 13 Sitting 10 Union Affairs Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira na Muungano 139 2023-11-10

Name

Maryam Azan Mwinyi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Chake Chake

Primary Question

MHE. MARYAM AZAN MWINYI aliuliza: -

Je, kuna mkakati gani kuhakikisha NEMC na ZEMA zinasajiliwa kwenye Mfuko wa GCF?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA alijibu:-

Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Maryam Azan Mwinyi, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, mkakati uliopo ni kuhakikisha NEMC, ZEMA pamoja na taasisi nyingine zilizoomba au zitakazoomba usajili chini ya GCF zinapata usajili katika Mfuko wa GCF. Hivyo, kwa sasa Serikali inaendelea na mawasiliano, majadiliano na mazungumzo ya kuhakikisha usajili kwa taasisi mbalimbali za Serikali unakamilika.

Mheshimiwa Spika, NEMC tayari imeshaomba na kuanza mchakato wa usajili (accreditation) tangu mwaka 2021, na kwa upande wa ZEMA ilikuwa bado haijawasilisha maombi ya usajili kwenye Mfuko wa GCF. Hata hivyo, Serikali itaendelea kuhakikisha taasisi zote zilizoomba usajili katika Mfuko wa GCF zinapata usajili ili kunufaika na faida za mfuko huo, ahsante sana.