Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Maryam Azan Mwinyi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Chake Chake

Primary Question

MHE. MARYAM AZAN MWINYI aliuliza: - Je, kuna mkakati gani kuhakikisha NEMC na ZEMA zinasajiliwa kwenye Mfuko wa GCF?

Supplementary Question 1

MHE. MARYAM AZAN MWINYI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa majibu mazuri ya Serikali. Nina maswali mawili ya nyongeza.

Je, ni hatua gani zinazotumika mpaka uungwe kwenye Mfuko huu wa GCF?

Swali la pili, kutokana na uhitaji wa miradi ya mazingira Zanzibar; je, ni lini ZEMA wataanza mchakato wa usajili kwenye Mfuko wa GCF? Ahsante. (Makofi)

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Dada yangu Mheshimiwa Maryam Azan Mwinyi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, hatua zilizokuwepo ni kwamba taasisi mbalimbali nchini mwetu ambazo Ofisi ya Makamu wa Rais ni mratibu zinawasilisha nia hiyo na mwishowe mchakato huo unaenda sasa katika mfuko huo. Mwisho wa siku ni kwamba, taasisi hiyo baada ya mchakato utakapokamilika basi inakuwa imekidhi viwango.

Mheshimiwa Spika, hata hivyo kumekuwa na changamoto katika mchakato huo kwa sababu zaidi ya taasisi sita nilizozipeleka hivi sasa bado hazijafanikiwa. Kwa hiyo, tumeendelea kufanya kazi hii kubwa ya kuhamasisha jinsi gani wenzetu waweze kukubali maombi yetu, kwa lengo kwamba taasisi zetu ziweze kunufaika.
Mheshimiwa Spika, upande wa swali la pili ni kweli, upande wa Zanzibar kuna changamoto kubwa za kimazingira. Hata hivyo, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira kwa kushirikiana na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, chini ya Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais, inaendelea kushirikiana kwa dhati.

Mheshimiwa Spika, naomba niwahakikishie Waheshimiwa Wabunge ni kwamba hivi sasa tunatekeleza baadhi ya miradi. Kwa mfano, ukienda kule Sipwese - Pemba, tunajenga ukuta pale wa Bahari, ukienda Kaskazini A na maeneo mbalimbali. Naomba niwahakikishie Waheshimiwa Wabunge kwamba tutaendelea kushirikiana lengo kubwa ni pande zote mbili za Muungano ziweze kupata fursa miradi maendeleo hususani katika hususan katika sekta hii ya mazingira, ahsante sana. (Makofi)