Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 13 Sitting 10 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 141 2023-11-10

Name

Conchesta Leonce Rwamlaza

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. CONCHESTA L. RWAMLAZA aliuliza: -

Je, lini Serikali itakamilisha jengo la Makazi ya Askari Polisi lililopo Kata ya Buyekera Bukoba?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu,

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Conchesta Leonce Rwamlaza, Mbunge Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali imetenga jumla ya shilingi bilioni moja kutoka kwenye bajeti ya mwaka wa fedha wa 2023/2024 kwa ajili ya kumalizia ujenzi wa jengo la makazi ya Askari Polisi lililopo Buyekera - Bukoba Mjini. Ujenzi huo unatarajiwa kuanza mara baada ya Wizara ya Fedha kuhamishia fedha hizo Jeshi la Polisi.