Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Conchesta Leonce Rwamlaza

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. CONCHESTA L. RWAMLAZA aliuliza: - Je, lini Serikali itakamilisha jengo la Makazi ya Askari Polisi lililopo Kata ya Buyekera Bukoba?

Supplementary Question 1

MHE. CONCHESTA L. RWAMLAZA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Pamoja na majibu ya Waziri, jengo hili limeanza kujengwa tangu mwaka 2010 ni miaka 13 sasa.

Kwanza, niulize Serikali kwa nini imetelekeza jengo hili mpaka limekuwa gofu?

Mheshimiwa Spika, sasa kwa sababu Serikali imesema itatoa bilioni moja, mtupe commitment Serikali ili azma ya kujenga jengo hili iweze kutimia. Ni lini Serikali inakwenda kukamilisha jengo hili?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, ni lini Serikali itakamilisha jengo hili? Nimeeleza kwenye jibu la msingi kwamba ni pale tutakapopata fedha zilizotengwa kwenye bajeti ya mwaka huu kwa ajili ya ukamilishaji.

Mheshimiwa Spika, nikuhakikishie tu Mheshimiwa siyo dhamira ya Serikali kuacha majengo kuwa magofu, majengo mengine yalitegemea uwepo wa fedha pale ambapo tulikwama na umesema ni miaka 10 iliyopita, ndiyo maana majengo mengi sasa hivi tunayakamilisha. Ukienda maeneo mbalimbali Geita Jengo la Polisi la Mkoa linakaribia kukamilika, Mara linakaribia, Njombe limekaribia kukamilika. Kwa hiyo, tuna imani Wizara ya Fedha itakapotoa fedha hizi ili jengo la Kagera pia tutalikamilisha. ahsante sana. (Makofi)

Name

Suma Ikenda Fyandomo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. CONCHESTA L. RWAMLAZA aliuliza: - Je, lini Serikali itakamilisha jengo la Makazi ya Askari Polisi lililopo Kata ya Buyekera Bukoba?

Supplementary Question 2

MHE. SUMA I. FYANDOMO: Mheshimiwa Spika, ahsante. Eneo la Ikuti Wilayani Rungwe kijiografia lipo mbali sana na Makao Makuu ya Wilaya ya Rungwe.

Sasa je, ni lini Serikali itajenga Kituo cha Polisi maeneo ya Ikuti, ili kuwaepushia shida wanayoipata kwa sasa? (Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, eneo la Ikuti ambalo ametuambia Mheshimiwa Mbunge lipo mbali sana na eneo Makao Makuu ya Wilaya ya Rungwe, anapendekeza tujenge jengo la Polisi pale na ndiyo dhamira ya Serikali. Kama utakuwa umefatilia hotuba ya Waziri wa Fedha mwaka huu, tumesema tunataka kujenga vituo vya Polisi karibu kila Kata. Tayari Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi imezungumza na TAMISEMI kuhusu mikakati ya kujenga vituo hivyo imeanza kufanyiwa kazi.

Mheshimiwa Spika, ni matarajio yetu kwamba, eneo hili la Ikuti - Rungwe ni moja ya maeneo yatakayonufaika na mpango huu, ahsante. (Makofi)

Name

Dorothy George Kilave

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Temeke

Primary Question

MHE. CONCHESTA L. RWAMLAZA aliuliza: - Je, lini Serikali itakamilisha jengo la Makazi ya Askari Polisi lililopo Kata ya Buyekera Bukoba?

Supplementary Question 3

MHE. DOROTHY G. KILAVE: Mheshimiwa Spika, ahsante.

Je, ni lini sasa Serikali mtaendeleza kujenga nyumba za askari pale Kilwa Road Barracks? Kwa sababu majengo mengine yamejengwa lakini mengine bado hayajaendelezwa. Naomba kujua sasa. (Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, tunatambua uchakavu wa baadhi ya majengo ya Makazi Jeshi la Polisi pale Kilwa Barracks. Ni mpango wa Serikali kama ambavyo tumeanza kujenga zile flats ambazo Mheshimiwa Mbunge ameziona, dhamira ya Serikali ni kuendelea hatua kwa hatua kadri ya upatikanaji wa fedha.

Mheshimiwa Spika, umesikia ikielezwa hapa kwamba tumefanya Dar es Salaam lakini maeneo mengine bado yanalia. Katika hali ya kutaka ku-balance kadri tutakavyofikiwa basi Dar es Salaam tutaiendeleza kadhalika pia.

Name

Sophia Hebron Mwakagenda

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. CONCHESTA L. RWAMLAZA aliuliza: - Je, lini Serikali itakamilisha jengo la Makazi ya Askari Polisi lililopo Kata ya Buyekera Bukoba?

Supplementary Question 4

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Waziri katika Jimbo la Busokelo, Kituo cha Polisi wanachotumia ni lililokuwa Jengo la Posta; ni lini mtaweka kituo kizuri ambacho kitasaidia huduma ya wananchi katika Jimbo lile? (Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, tunafahamu changamoto ya maeneo mapya ya utawala ambayo yanaanzishwa kwa dhamira njema ya kusogeza huduma kwa wananchi, ikiwa ni pamoja na huduma za usalama, ndiyo maana wakati maeneo haya yakianza wenyeji kwa maana ya wenye maeneo Wilaya husika walibainisha, kama tukianzisha Makao Makuu Wilaya mpya huduma hii itafanyikia wapi? Kwa kutambua changamoto hiyo, ndiyo maana Wizara ya Mambo ya Ndani imeshabaini Wilaya zote ambazo hazina vituo vya ngazi ya Wilaya vya Polisi na tunaendelea kujenga kadri fedha zinavyopatikana.

Mheshimiwa Spika, ninakuahidi Mheshimiwa Mwakagenda kwamba, Busokelo litakuwa ni eneo pia litakalotiliwa maanani tunavyoendelea kutekeleza mpango wetu, ahsante sana.

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. CONCHESTA L. RWAMLAZA aliuliza: - Je, lini Serikali itakamilisha jengo la Makazi ya Askari Polisi lililopo Kata ya Buyekera Bukoba?

Supplementary Question 5

MHE. SUBIRA K. MGALU: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi kuuliza swali la nyongeza.

Kwa kuwa, Serikali imejenga majengo mazuri sana ya Makao Makuu ya Polisi katika Mkoa wa Kusini Unguja, Tunguu na Mkoa wa Kaskazini Unguja na yamezinduliwa, tuliyashuhudia katika ziara ya Mheshimiwa Mwenyekiti wa UWT Taifa. Je, ni lini sasa majengo haya yatapatiwa samani ili yaanze kutumika kutokana na uwekezaji mkubwa mliofanya Serikali wa zaidi ya shilingi bilioni tatu? Ahsante sana.

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa Mbunge kutambua juhudi ambazo zimefanywa na Serikali ya Dkt. Samia Suluhu Hassan, katika kutengeneza mazingira ya kutolea huduma za kiusalama yakiwemo majengo ya Polisi ngazi ya Mkoa na Wilaya.

Mheshimiwa Spika, ni kweli ujenzi ni hatua, kukamilisha majengo ni jambo moja na uwekaji wa samani ni jambo la pili. Hatua itakayofuata ni kuruhusu majengo yaanze kutumika na Jeshi la Polisi limejipanga vema katika bajeti yake ya mwaka huu kuyapatia samani majengo hayo, yakiwemo hayo ya Tunguu na Kusini Unguja. Nashukuru.