Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 13 Sitting 10 Defence and National Service Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga taifa 142 2023-11-10

Name

Maimuna Ahmad Pathan

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MAIMUNA A. PATHAN aliuliza: -

Je, lini Serikali itawalipa fidia wananchi waliopisha upanuzi wa maeneo ya Jeshi 843 KJ Nachingwea?

Name

Dr. Stergomena Lawrence Tax

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI K.n.y. WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Maimuna Ahmad Pathan, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Kikosi cha Jeshi cha 843 JKT Nachingwea, kilichopo Mkoani Lindi kilianzishwa mwaka 1964. Kumbukumbu zinaonesha eneo husika lilikuwa ni moja ya mashamba ya karanga yaliyokuwa yanamilikiwa na Mzungu aliefahamika kwa majina ya John Molam. Shamba hilo baadae lilitaifishwa na Serikali na kutumika kwa matumizi ya Kijeshi kwa ajili ya kuimarisha Ulinzi katika mipaka ya Kusini mwa Tanzania.

Mheshimiwa Spika, mwaka 1964 wakati Jeshi wanakabidhiwa eneo hilo, upande wa mpaka wa Mashariki kikosi kilipakana na Kijiji cha Naipingo, baadaye eneo la Jeshi katika mpaka wa upande huo lilikatwa na kuanzishwa Kijiji cha Mkukwe ambacho kilisajiliwa Mwaka 1999. Kwa sasa kikosi kinapakana na Kijiji cha Mkukwe katika upande huo wa Mashariki. Upimaji mpya wa kurekebisha mipaka uliofanyika mwaka 2021 na Hatimiliki yake imetolewa 2023.

Mheshimiwa Spika, kwa mantiki hiyo hakuna upanuzi uliofanywa wa kuongeza eneo la kikosi, bali eneo la Jeshi ndilo lilipunguzwa na kuanzisha kijiji cha Mkukwe Mwaka 1999. Nashukuru.