Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Maimuna Ahmad Pathan

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MAIMUNA A. PATHAN aliuliza: - Je, lini Serikali itawalipa fidia wananchi waliopisha upanuzi wa maeneo ya Jeshi 843 KJ Nachingwea?

Supplementary Question 1

MHE. MAIMUNA A. PATHAN: Mheshimiwa Spika, ahsante, swali langu la kwanza la nyongeza ni kwamba Kikosi cha 41 KJ Nachingwea pia kuna maeneo yalitwaliwa na Jeshi. Ni maeneo ambayo wazee wetu waliyatunza miaka mingi sana.
Je, Serikali haioni haja ya kuwalipa fidia wazee hao?

Swali la pili, kwa kuwa wazee waliyatunza maeneo yote hayo kwa muda mrefu na ilikuwa ni tegemeo kwa maisha yao. Je, Serikali haioni haja kweli ya kuwalipa hata kifuta jasho kidogo ili maisha yaendelee? (Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, kwa mujibu wa swali la msingi nililolijibu inaonesha kwamba hakuna mgogoro, lakini kwa swali la nyongeza aliloliuliza Mheshimiwa Mbunge Pathan, naomba nilichukue ili kuelekeza Jeshi la Wananchi wa Tanzania, Kikosi cha 41 KJ, walifuatilie na kuleta taarifa stahiki ili hatua stahiki ziweze kuchukuliwa. Nashukuru. (Makofi)

Name

Noah Lemburis Saputi Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Magharibi

Primary Question

MHE. MAIMUNA A. PATHAN aliuliza: - Je, lini Serikali itawalipa fidia wananchi waliopisha upanuzi wa maeneo ya Jeshi 843 KJ Nachingwea?

Supplementary Question 2

MHE. NOAH L. S. MOLLEL: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi.

Mheshimiwa Spika, wananchi wa Kata ya Oldonyosambu wamechukuliwa maeneo yao na Jeshi miaka 20 sasa imepita na zaidi. Je, ni lini itawalipa fidia wananchi wale ambao wametoa eneo lao katika Kata ya Oldonyosambu?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, kwenye hili la Oldonyosambu pia ni suala jipya kwangu. Kama Naibu Waziri niliyeshikilia jambo hili, naomba nilichukue ili tuwasiliane na Waziri mwenye dhamana na chombo chenyewe cha jeshi, kuona uhalali. Kama ambavyo tumesema wakati wote, Serikali ya Awamu ya Sita ya Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, haiko tayari kuona wananchi wake wakidhulumiwa au kunyimwa haki wanayostahili.
Mheshimiwa Spika, ikithibitika kwamba wanastahili kulipwa fidia, basi hatua stahiki zitachukuliwa ili wananchi hawa waweze kulipwa inavyopasa, nashukuru.