Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 13 Sitting 10 Water and Irrigation Wizara ya Maji 143 2023-11-10

Name

Miraji Jumanne Mtaturu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Mashariki

Primary Question

MHE. MIRAJI J. MTATURU aliuliza:-

Je, lini Serikali itachimba Mabwawa ya maji Kata za Kikio, Misughaa, Lighwa, Mungaa, Siuyu, Issuna na Mkiwa – Singida?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Miraji Jumanne Mtaturu, Mbunge wa Jimbo la Singida Mashariki, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Wilaya ya Ikungi ina jumla ya kata 28 zikiwemo Kata za Kikio, Misughaa, Lighwa, Mungaa, Siuyu, Issuna na Mkiwa. Vyanzo vikuu vya maji katika kata hizo ni maji chini ya ardhi kupitia visima vilivyochimbwa na kuwekewa miundombinu ya kutolea maji. Vijiji vyote vya Kata za Mungaa, Siuyu, Issuna na Mkiwa vinapata huduma ya maji kwa kutumia visima vilivyochimbwa kwenye vijiji hivyo. Aidha, baadhi ya vijiji katika Kata za Kikio, Misughaa na Lighwa bado havijapatiwa huduma ya maji ya kutosheleza.

Mheshimiwa Spika, katika kuhakikisha huduma ya majisafi na usafi wa mazingira zinatosheleza katika Wilaya ya Ikungi Ikiwemo Kata za Kikio, Misughaa, Lighwa, Mungaa, Siuyu, Issuna na Mkiwa, Serikali imeandaa Mpango Mkakati wa Miaka Mitano kuanzia 2022/2023 – 2025/2026 wa kujenga mabwawa ya kuvuna maji ya mvua ili yatumike wakati wa kiangazi sambamba na kudhibiti mafuriko. Mwaka 2024/2025 itafanya usanifu wa kina na kubaini maeneo yanayofaa kwa ajili ya ujenzi wa mabwawa katika kata hizo.