Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Miraji Jumanne Mtaturu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Mashariki

Primary Question

MHE. MIRAJI J. MTATURU aliuliza:- Je, lini Serikali itachimba Mabwawa ya maji Kata za Kikio, Misughaa, Lighwa, Mungaa, Siuyu, Issuna na Mkiwa – Singida?

Supplementary Question 1

MHE. MIRAJI J. MTATURU: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Namshukuru sana Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu ya Serikali. Sasa nina maswali mawili ya nyongeza:-

Mheshimiwa Spika, mpaka sasa coverage ya maji katika Wilaya ya Ikungi ni asilimia 53 ambayo iko chini sana, kuna maeneo ambayo yana changamoto kubwa. Sasa nataka tu nijue, ni nini mpango wa Serikali wa muda mfupi kuwapatia maji wananchi wa Wilaya ya Ikungi kwa maana ya Kata za Kikio katika Kijiji cha Nkundi, Lighwa katika Kijiji cha Mwisi na Issuna katika Kijiji cha Issuna A, Kitongoji cha Manjaru?

Mheshimiwa Spika, swali la pili. Kuna visima vilivyochimbwa ambavyo bado havijawekewa miundombinu. Nilitaka nijue kwamba, visima hivyo katika vijiji vya Msule, Mkinya, Mang’onyi na Mbwanchiki pamoja na Ujaire.

Ni lini sasa Serikali itatenga fedha ya kujenga miundombinu ili kuondoa adha ya maji katika maeneo haya niliyoyataja? (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, mpango wa muda mfupi kwenye kata na vijiji alivyovitaja Mheshimiwa Mtaturu, ni kwamba tutaendelea kufanya jitihada za kuhakikisha tunakuja kuchimba visima.

Mheshimiwa Spika, naomba nitumie Bunge lako Tukufu nimwagize RM Singida, ahahakikishe anakwenda kwenye hizi kata, wafanye usanifu ili kuona wapi tunaweza tukapata maji chini ya ardhi ili sasa waweze kupelekewa gari wakachimbe visima na wananchi waweze kupata huduma ya maji safi na salama.

Mheshimiwa Spika, swali lake la pili, lini tutatenga fedha kwa ajili ya miundombinu kwenye visima tulivyochimba; kwa utaratibu wa Wizara, tukishachimba visima kazi inayofuata ni usambazaji. Kwa hiyo, nina uhakika kama mwaka huu wa fedha kwa maana ya kuanzia leo mpaka Juni, Wizara tukawa tumepata fedha ambazo hazitoshelezi kuwafikia, mwaka ujao wa fedha lazima maeneo haya yote tuje tusambaze maji katika visima ambavyo tumevichimba.

Name

Esther Lukago Midimu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MIRAJI J. MTATURU aliuliza:- Je, lini Serikali itachimba Mabwawa ya maji Kata za Kikio, Misughaa, Lighwa, Mungaa, Siuyu, Issuna na Mkiwa – Singida?

Supplementary Question 2

MHE. ESTHER L. MIDIMU: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi hii niweze kuuliza swali la nyongeza. Mabwawa mawili, Bwawa la Luguru na Bwawa la Mwamapalala, Wilaya ya Itilima, Mkoa wa Simiyu yana hali mbaya, yamejaa tope: Je, ni lini Serikali itafanya ukarabati wa mabwawa hayo? (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Esther Midimu, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, mabwawa haya aliyoyataja niseme tu kwamba, tuko kwenye utaratibu wa kuona kama tutaweza kuendelea kuyatumia tuje tuweze kuyakarabati. Pia kwa Mkoa wa Simiyu tuna mradi mkubwa sana ambao unakwenda kutatua changamoto ya maji katika maeneo haya mengi. Kwa hiyo, huenda tusikarabati, lakini tukautumia mradi ule wa mabadiliko ya tabianchi kuhakikisha maeneo haya aliyoyataja Mheshimiwa Mbunge tunayapelekea maji safi na salama. (Makofi)

Name

Kiswaga Boniventura Destery

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Magu

Primary Question

MHE. MIRAJI J. MTATURU aliuliza:- Je, lini Serikali itachimba Mabwawa ya maji Kata za Kikio, Misughaa, Lighwa, Mungaa, Siuyu, Issuna na Mkiwa – Singida?

Supplementary Question 3

MHE. BONIVENTURA D. KISWAGA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Kwa kuwa Mji wa Kisesa na Bujora una hali mbaya sana ya upatikanaji wa maji; na kwa kuwa Serikali imetoa fedha kujenga tank kubwa la cubic meter milioni tano: Je, ni lini usabazaji wa mabomba utaanza katika Mji wa Kisesa na Bujora?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Boniventura Kiswaga, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni kweli, maeneo aliyoyataja Mheshimiwa Mbunge yapo kwenye mchakato wa utekelezaji wa mradi mkubwa ambao huu Mji wa Kisesa tayari mabomba makubwa ya nchi 10 yameshaanza kulazwa kama kilometa tatu hivi, lakini tayari mabomba ya nchi nane pia yako pale site. Kwa hiyo, nimwondoe hofu Mheshimiwa Mbunge. Nimpongeze kwa kufuatilia, lakini hizi kazi tayari zimeanza, na amekiri tank kubwa linajengwa pale Bujora, na penyewe pia utaratibu unaendelea wa kuongeza mabomba ambayo yatatosheleza mradi huu mzima wa Kisesa na Bujora.

Name

Khadija Shaaban Taya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MIRAJI J. MTATURU aliuliza:- Je, lini Serikali itachimba Mabwawa ya maji Kata za Kikio, Misughaa, Lighwa, Mungaa, Siuyu, Issuna na Mkiwa – Singida?

Supplementary Question 4

MHE. KHADIJA S. TAYA: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana. Kutokana na tatizo la maji katika Wilaya hizi za Mkoa huu wa Dodoma, naomba niulize swali kwamba ni lini Bwawa la Farkwa litaanza ujenzi kama ilivyo katika mkakati wa Serikali? Ahsante. (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Khadija Taya, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, napenda kusema nina furaha kubwa sana kwa sababu, sasa ujenzi wa Bwawa la Farkwa upo tayari kwenye pipe. Ni wiki iliyopita tu wameweza kusaini mkataba wa kazi hii kuanza na tutarajie kazi itakwenda vizuri kwa sababu ni mradi ambao tunautarajia sana katika kupunguza changamoto ya maji kwenye Jiji la Dodoma. (Makofi)