Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 13 Sitting 10 Works and Transport Wizara ya Uchukuzi 148 2023-11-10

Name

Mashimba Mashauri Ndaki

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Magharibi

Primary Question

MHE. MASHIMBA M. NDAKI aliuliza: -

Je, Mkandarasi wa SGR kipande cha Seke-Malampaka hadi Malya ameajiri wananchi wangapi wanaotoka maeneo hayo?

Name

David Mwakiposa Kihenzile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Uchukuzi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mashimba Mashauri Ndaki, Mbunge wa Maswa Magharibi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia TRC imeendelea kumuelekeza mkandarasi wa ujenzi wa reli ya SGR, kuendelea kutoa ajira kwa wananchi wanaopitiwa na mradi, sambamba na kufuata taratibu na sheria za ajira nchini. Aidha, Serikali imeendelea kutekeleza ujenzi wa SGR kipande cha Mwanza - Isaka (kilometa 341), kinachojumuisha kipande cha Seke - Malampaka hadi Malya kama sehemu ya mradi huo.

Mheshimiwa Spika, kuhusu ajira; hadi kufikia mwishoni mwezi Agosti 2023, mkandarasi ameajiri jumla ya wananchi 6,793. Kati ya hao, wananchi 1,639 kutoka Mkoa wa Shinyanga, wananchi 1,973 kutoka Mkoa wa Mwanza, wananchi 525 kutoka Mkoa wa Simiyu, wananchi 352 kutoka mkoa wa Tabora na wanachi 2,304 kutoka mikoa mingine.

Mheshimiwa Spika, Serikali itaendelea kumsimamia Mkandarasi kuhakikisha kuwa anaajiri kwa kutoa kipaumbele kwanza kwa wananchi wa maeneo husika kabla ya kutafuta ujuzi stahiki kutoka maeneo mengine.