Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 13 Sitting 10 Health and Social Welfare Wizara ya Afya 149 2023-11-10

Name

Constantine John Kanyasu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Primary Question

MHE. CONSTANTINE J. KANYASU aliuliza: -

Je, kwa nini NHIF inazuia matibabu ya baadhi ya wagonjwa wenye Bima za Afya wakiwa hospitali?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Afya naomba kujibu swali la Mheshimiwa Constantine John Kanyasu, Mbunge wa Geita, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kulikuwa na zoezi la uhakiki wa uhalali wa wanufaika wa Mfuko wa Bima ya Afya. Zoezi hilo lilileta usumbufu ambao ungeweza kuzuilika kama wahakiki hao wangetumika wataalamu wenye miiko ya taaluma ya tiba. Wizara ilipopata malalamiko hayo ilifuatilia mara moja na kufanya maboresho ambayo yaliyoondoa usumbufu kwa wateja.

Mheshimiwa Spika, nitumie nafasi hii kuielekeza Menejimenti ya Mfuko wa Bima ya Afya katika kipindi cha miezi mitatu, ihakikishe inaboresha mifumo ya TEHAMA itakayoweza kuondoa usumbufu na pia kudhibiti udanganyifu pasipo kuwa kero kwa wanufaika wa Mfuko, naomba kuwasilisha.