Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 13 Sitting 10 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi 151 2023-11-10

Name

Hussein Nassor Amar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyang'hwale

Primary Question

MHE. HUSSEIN N. AMAR aliuliza: -

Je, ni lini upembuzi yakinifu utakamilika na kuanza ujenzi wa barabara ya Kahama – Nyang’hwale – Busisi?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Ujenzi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Hussein Nassor Amar, Mbunge wa Nyang’hwale, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, zabuni ya manunuzi kwa ajili ya kumpata Mhandisi Mshauri wa kufanya kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa barabara ya Kahama, Nyang’hwale hadi Busisi yenye urefu wa kilometa 162.9, inatarajiwa kukamilika mwishoni mwa mwezi Februari 2024. Kazi za upembuzi yakinifu na usanifu wa kina zinatarajiwa kuchukua muda wa mwaka mmoja. Hivyo kazi zitakamilika mwezi Februari, 2025. Baada ya usanifu kukamilika na gharama za ujenzi kujulikana, Serikali itatafuta fedha kwa ajili ya kuanza ujenzi, ahsante.