Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 13 Sitting 10 Community Development, Gender and Children Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum 154 2023-11-10

Name

Janeth Elias Mahawanga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JANETH E. MAHAWANGA aliuliza: -

Je, Serikali ina mkakati gani kuhamasisha watoto wadogo kukua katika misingi ya kutambua madhara ya ukatili wa kijinsia?

Name

Mwanaidi Ali Khamis

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUM alijibu:-

Mheshimiwa Spika, ahsante, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsi, Wanawake na Makundi Maalum, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Janeth Elias Mahawanga, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali imeandaa mwongozo wa Taifa wa uundaji na uendeshaji wa Mabaraza ya Watoto ya mwaka 2022, ambapo hadi Juni 2023, jumla ya Mabaraza ya Watoto 651 yameanzishwa kwenye ngazi za mitaa katika mikoa 12 ya Tanzania Bara.

Mheshimiwa Spika, katika mabaraza haya, watoto wamejifunza mbinu na stadi za maisha zinazowapa ufahamu na viashiria vya ukatili. Aidha, katika Mabaraza ya Watoto wanajifunza kujieleza, kujiamini na kujisimamia katika masuala yanayowahusu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Serikali pia imewezesha uandaaji wa mwongozo wa Taifa wa dawati la ulinzi na usalama wa mtoto, ndani na nje ya shule wa mwaka 2022. Mwongozo huu unahimiza watoto wenyewe kushiriki katika ulinzi wao na kutoa taarifa ya vitendo vya ukatili vinavyotokea shuleni, njiani na kuelekea nyumbani na vyumbani, ahsante. (Makofi)