Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Janeth Elias Mahawanga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JANETH E. MAHAWANGA aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani kuhamasisha watoto wadogo kukua katika misingi ya kutambua madhara ya ukatili wa kijinsia?

Supplementary Question 1

MHE. JANETH E. MAHAWANGA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali, lakini nina maswali madogo mawili ya nyongeza. Swali la kwanza. ukiacha mikoa 12 ya Tanzania Bara ambayo imefanikiwa kupata haya Mabaraza ya Watoto, nini mkakati wa Serikali kuhakikisha mikoa 14 iliyobaki nayo inapata mabaraza haya? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili; suala la vitendo vya ukatili kwa watoto limekuwa likiendelea siku hadi siku kwenye jamii yetu. Je, Serikali haioni haja sasa yakuja na sheria kali itakayo komesha vitendo hivi? Ahsante. (Makofi)

Name

Mwanaidi Ali Khamis

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII, JINSI, WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUM: Mheshimiwa Spika, ahsante. Napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali imepanga kuanzisha mabaraza haya katika shule zote za vijijini na mitaani nchi nzima. Serikali pia imeshasambaza Mwongozo wa Taifa wa uwaandaaji na uendeshaji wa Mabaraza ya Watoto katika halmashauri zote nchini, ambapo utawasaidia kuendesha mabaraza hayo kwa kushirikiana na Maafisa wa Maendeleo ya Jamii na Maafisa Ustawi wa Jamii.

Mheshimiwa Spika, swali lake la pili, Bunge lako Tukufu limeshapitisha sheria na adhabu kali za kukomesha vitendo vya ukatili kwa watoto. Niwaombe wananchi, waendelee kutoa ushirikiano kwa Maafisa Mahakama na kutoa ukweli pale wanapofika katika sheria. Niwasisitize kuwa, mahakama itaendelea kufanya kazi yake pale ukweli watakapoutoa katika sehemu za sheria, ahsante. (Makofi)