Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 4 Sitting 4 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 47 2016-09-09

Name

Lathifah Hassan Chande

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. CECIL D. MWAMBE (K.n.y. MHE. LATHIFAH H. CHANDE) aliuliza:-
Mji wa Liwale umebakia kuwa ni Wilaya pekee ya Mkoa wa Lindi ambayo haijanufaika na umeme wa uhakika wa gesi asilia. Umeme unaotumika ni wa jenereta mbili za diseli za kW 800:-
Je, ni kwa nini Serikali isitenge fedha ili kuiunganisha Wilaya nzima ya Liwale na umeme wa gesi asilia?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nishati na Madini, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Lathifah Hassan Chande, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Mji wa Liwale unapata umeme kutoka Kituo cha Kuzalisha umeme kwa kutumia mafuta kilichopo Liwale. Hata hivyo, gharama za uendeshaji wa mitambo hiyo inayotumia nishati ya mafuta ni kubwa sana. Kutokana na hali hiyo, Serikali imeanza kutekeleza ujenzi wa njia ya umeme itakayounganisha Wilaya ya Liwale na Wilaya ya Nachingwea ambayo kwa sasa inatumia umeme kutoka Kituo cha Kuzalisha umeme cha Gesi Asilia kilichopo Mtwara.
Mheshimiwa Naibu Spika, hatua iliyofikiwa katika mpango huo ni ujenzi wa njia ya umeme wa msongo wa kilovoti 33 yenye urefu wa kilometa 14.5 kutoka Nachingwea hadi Kijiji cha Luponda, ambapo ni kilometa 73 kutoka Liwale hadi Kijiji cha Nangano. Kazi hiyo, ilianza mwezi Agosti mwaka 2014 na inatarajiwa kukamilika mwishoni mwa Septemba mwaka huu. Gharama za mradi huu ni shilingi bilioni 3.5 na kwa kweli, inaendelea vizuri. Hata hivyo, sehemu iliyobaki ya kilometa 45 kati ya Luponda na Nangano inatarajiwa kukamilika kupitia utekelezaji wa Mpango wa REA awamu ya tatu.