Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 53 Health and Social Welfare Wizara ya Afya 465 2022-06-28

Name

Abdallah Dadi Chikota

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nanyamba

Primary Question

MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itapeleka Watumishi wa kutosha katika Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Kusini iliyopo Mtwara?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Afya, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Abdallah Dadi Chikota, Mbunge wa Nanyamba, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mtwara ilizinduliwa mwezi Oktoba, 2021 ikiwa na watumishi 45. Kwenye kibali cha sasa cha ajira imepangiwa watumishi wapya 112 itakayofanya idadi ya watumishi kufikia 157 mwezi Julai, 2022, ahsante.