Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 53 Health and Social Welfare Wizara ya Afya 466 2022-06-28

Name

Jesca Jonathani Msambatavangu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Iringa Mjini

Primary Question

MHE. JESCA J. MSAMBATAVANGU aliuliza:-

Je, ni lini ombi la kubadilishana Hospitali ya Mkoa na ya Wilaya litafanyiwa kazi kuruhusu upanuzi wa Hospitali ya Mkoa wa Iringa?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Afya, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Jesca Msambatavangu, Mbunge wa Iringa Mjini kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali imepokea ushauri wa Mheshimiwa Mbunge, hivyo mwezi Julai 2022 timu ya wataalamu itakwenda Mkoani Iringa ili kuja na ushauri wa kitaalamu wa namna ya kutekeleza suala hili bila kuathiri mfumo wa utoaji wa huduma za afya katika Mkoa, ahsante.