Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 53 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 467 2022-06-28

Name

Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Primary Question

MHE. AIDA J. KHENANI aliuliza:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kupitia upya mipaka ya hifadhi na makazi ya wananchi Wilayani Nkasi?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-

Mheshimiwa Spika, ahsante, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Aida Joseph Khenani, Mbunge wa Nkasi, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali imeanza kutatua changamoto hiyo kwa kuweka vigingi ambapo hadi sasa jumla ya vigingi 111 vimewekwa kati ya vigingi 322 vinavyohitajika. Zoezi hili linaendelea hata kwa mwaka wa fedha 2022/2023 ambapo vigingi vilivyobaki vitawekwa. Serikali itaendelea na jitihada za kutoa elimu kwa wananchi kuhusu namna ya kutambua na kuheshimu mipaka ya hifadhi.