Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 53 Finance and Planning Wizara ya Fedha na Mipango 469 2022-06-28

Name

Juma Usonge Hamad

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chaani

Primary Question

MHE. JUMA USONGE HAMAD aliuliza:-

Je, kuna mpango gani wa kupunguza kodi, tozo na ushuru wa bidhaa za chakula/mboga kutoka Tanzania Bara kwenda Zanzibar?

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO alijibu:-

Mheshimiwa Spika, ahsante, kwa niaba ya Waziri wa Fedha na Mipango, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Juma Usonge Hamad, Mbunge wa Chaani, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, bidhaa za chakula na mbogamboga halisi zinazotoka Tanzania Bara kwenda Zanzibar hazitozwi kodi, tozo na ushuru wa aina yoyote kwa mujibu wa sheria, lakini bidhaa za chakula kutoka viwandani hutozwa tozo ya uchakataji nyaraka za forodha ya asilimia 0.6 tu kwenye thamani ya mzigo huo. Lengo la tozo hii ni kugharamia huduma ya uchakataji wa nyaraka za forodha na hutozwa kwa wateja wote wanaotumia mfumo wa forodha.

Mheshimiwa Spika, bidhaa za chakula na mbogamboga halisi hazitozwi tozo ya uchakataji wa nyaraka kwa sababu, hazihitaji kufanyiwa mchakato wa nyaraka katika mfumo wa forodha, ahsante.