Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Juma Usonge Hamad

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chaani

Primary Question

MHE. JUMA USONGE HAMAD aliuliza:- Je, kuna mpango gani wa kupunguza kodi, tozo na ushuru wa bidhaa za chakula/mboga kutoka Tanzania Bara kwenda Zanzibar?

Supplementary Question 1

MHE. JUMA USONGE HAMAD: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa fursa ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa bidhaa ambazo tayari za mifugo hususan ng’ombe pamoja na mbuzi kwa Zanzibar ni adimu sana, lakini pia bei yake inakuwa ni ghali sana. Je, Serikali ina mpango gani sasa wa kuhakikisha kwamba kufuta, lakini pia kupunguza kodi zote zile ambazo zinakuwa-charged pale bandarini kwa upande wa Tanga pamoja na Kitumbwi, bandari ya Tanga ili sasa kumpunguzia Mtanzania wa Zanzibar gharama nafuu bidhaa ile ya ng’ombe kama wa Bara?

Mheshimiwa Spika, lakini swali la pili; je, ni lini hasa Mheshimiwa Waziri utapanga safari ya kwenda bandarini kwenda kushuhudia namna Watanzania wanavyolazimishwa kulipa kodi maeneo ya bandarini? Ahsante. (Makofi)

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Juma Usonge Hamad kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, suala la usafirishaji wa nyama za mbuzi, ng’ombe na wanyama wengine ni kweli kwamba kupeleka Zanzibar ni nyama adimu hazipatikani sana, lazima tunavusha kutoka bara kwenda kule. Lakini suala la ufuataji wa kodi na tozo naomba hili tulichukue tulifanyie mchakato kwa sababu ni suala la kisheria.

Mheshimiwa Spika, swali lake la pili kuhusu kwenda kutembelea ili kuona hali halisi naomba niambatane mimi na yeye mara tu Bunge hili litakapomalizika tuende tukatembelee katika sehemu husika. (Makofi)