Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 53 Water and Irrigation Wizara ya Maji 472 2022-06-28

Name

Dr. Jasson Samson Rweikiza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Vijijini

Primary Question

MHE. DKT. JASSON S. RWEIKIZA aliuliza:-

Je, ni lini ujenzi wa Mradi wa Maji Kemondo - Maruku katika Jimbo la Bukoba Vijijini utakamilika.

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Maji naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Jasson Samson Rweikiza Mbunge wa Jimbo la Bukoba Vijijini kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2021/2022, Serikali inaendelea na utekelezaji wa awamu ya kwanza inayohusisha ujenzi wa chanzo cha maji na ulazaji wa bomba kuu kilometa nne na tenki la ujazo wa lita 3,000,000. Katika mwaka wa fedha 2022/2023 utekelezaji wa mradi utaendelea na unatarajiwa kukamilika mwezi Juni, 2023.

Mheshimiwa Spika, mradi huo utanufaisha Kata Tano za Bukoba Vijijini ambazo ni Kemondo, Bujogo, Katerero, Maruku na Kanyangereko.